Monday, November 25, 2013

Ndugu zangu wakulima, ni msimu wa kilimo sasa, mvua zimekwishaanza kunyesha maeneo mengi hapa nchini. Najua mkulima yuko bize kuhakikisha anapata pembejeo za kuweka shambani mwake.
Katika harakati hizo za kupata Mbolea na Mbegu bora, mkulima anapitia changamoto nyingi.

Katika soko la Pembejeo, mkulima anatapeliwa kwa kuuziwa mbolea na mbegu feki na wafanyabiashara wadanganyifu. Baada ya hapo mkulima anakuja kulia katika mavuno. Lakini haya yote wakubwa wenye mamlaka ya juu hawayajui? Na kama wanajua je, wameamua kwa makusudi kuwaacha waendelee na wizi huu? Kila mtu ajiulize swali hilo.

Tuache yote, hebu tuangalie sasa kumsaidia na kumshauri mkulima ili angalau aepuke kwa kiasi fulani kununua pembejeo feki na ambazo hazina kiwango.
Kwanza kabisa mkulima mwenyewe kabla hajanunua pembejeo ajiulize na kuamua, mbolea ama mbegu gani anahitaji kutumia na kulima. Katika kufanikisha hilo, mambo yafuatayo yanatakiwa mkulima kuzingatia:

1. Nunua pembejeo mahali stahiki yaani kwenye maduka maalumu ya pembejeo- Hili ni muhimu sana, wakulima wengi wanaotapeliwa ni kukosa umakini katika ununuzi wa pembejeo. Kutokana biashara huria tuliyonayo, mtu anaamua tu kuanza biashara ya pembejeo bila kufuata vigezo vinavyotakiwa. Kwa hiyo chunguza mazingira ya duka unalonunua pembejeo zako, je, yanaridhisha?

2. Unaponunua pembejeo yoyote ile, hakikisha unaomba list, hii itakusaidia endapo mambo yataharibika huko shambani. Hakikisia list hiyo inaeleza mambo muhimu kama Jina kamili la duka, mahali duka lilipo, mawasiliano na aina ya bidhaa uliyonunua.
3. Angalia muda wa mwisho kutumika (expire date) kwa pembejeo uliyonunua kabla hata hujaondoka dukani.

4. Unapotumia pembejeo yoyote ile hakikisha unabakiza walai kiasi kidogo kama ushahidi katika vipimo pale inapoonekana tofauti. Hii inamrahisishia mtaalam wa kilimo aliyekaribu kupata pa kuanzia pale panapotokea tatizo.

5. Epuka kununua pembejeo vichochoroni eti kisa zina bei rahisi.

Mambo hayo matano ni ya kuzingatia sana wakati wa ununuzi wa pembejeo. Nawatakia kilimo chema.��ba li

2 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete
  2. I wanna say thanks to DARK WEB for helping me boost my credit score from 420 to 840 excellent. Last year June i wasn't able to afford to pay my house rent due to my low credit score until i met dark web he help me erased all bad reports on my credit line, boost my credit score. I would advise y'all to get in touch with him if you have any issues with your credit score, just text him on his email; DARKWEBONLINEHACKERS@GMAIL.COM or his number (803) 392-1735

    ReplyDelete