Saturday, November 9, 2013

(i) NYANYA

(d) MAGONJWA YA NYANYA.
Kuna magonjwa mengi ambayo hushambulia sehemu zote za mmea wa nyanya. Baadhi ya magonjwa husababishwa na ukungu (fungus), vimelea (bacteria) na sumu (virus). Vile vile kuna magonjwa ya kunyauka au kuoza ambayo husababishwa na hali mbaya ya hewa . Magonjwa yaliyo mabaya sana ni:

1. Fusarium Wilt: Ugonjwa huu ni mbaya sana na husababisha mmea kudhoofu na majani kujikunjakunja. Rangi ya majani hugeuka njano, hatimaye kufa kuanzia chini kuelekea juu. Mimea iliyoambukizwa lazima ing'olewe na kuchomwa moto. Mpaka sasa haijapatikana dawa maalumu ya kuzuia ugonjwa huu. Kwa kuwa ukungu usababishao ugonjwa huu huishi ardhini, ni lazima kutibu udongo au kupanda aina zinazovumilia.

2. Bacteria Wilt:
Hustawi zaidi ktk hali ya joto. Mimea hudhoofu ghafla. Shina likikatwa hutoa ute mweupe na mzito. Vimelea visababishavyo ugonjwa huu huishi ardhini. Huzuiwa kwa kunyunyiziwa copper kila baada ya siku kumi. Mimea yote iliyoshambuliwa sharti ing'olewe na kuchomwa moto. Sehemu hiyo isipandwe nyanya, bilingani, pilipili au viazi mviringo kwa muda wa miaka minne ifuatayo.

3. Early Blight:
Huu ni ugonjwa wa kawaida lakini waweza kuleta hasara kubwa. Zaidi hushambuliwa miche na mimea michanga ambayo mashina yake huoza kwa chini. Majani hupata madoa ambayo huendelea kupanuka, na hatimaye baadhi ya majani hupukutika. Ni muhimu kutibu mbegu kabla ya kuzipanda. Dawa zenye asili ya copper au sulphur huweza kuzuia ugonjwa huu. Usipande mimea asili ya nyanya ktk eneo hilo.

4. Blossom - End Rot:
Huu ni ugonjwa wa matunda, husababishwa na hali mbaya ya hewa, hasa ukame. Huozesha robo hadi nusu ya tunda. Hutokea pia nyakati za mvua nyingi zifanyazo udongo kuwa tope. Kupunguza ugonjwa huu ni kuhakikisha kuwa ardhi ina unyevu wa kutosha wakati wa kupanda.

Pia kuna magonjwa mengi kama Leaf spot, Tomato Mosaic na Anthracnose.
Magonjwa yote yanaweza kuzuiwa kwa kupiga dawa za sumu kama Diathane M45, Thiodan n.k

(e) WADUDU.
Kuna aina nyingi, lakini wanazuiwa kwa kupiga madawa kama Thiodan, Malathion n.k ��mu ku

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete