Thursday, November 7, 2013

---------- Forwarded message ----------
From: mmisungwi@gmail.com
Date: Thu, 7 Nov 2013 21:08:00 +0400
Subject: MPANGO WA MIKOPO YA PEMBEJEO.
To: misungwi.mgonga@blogger.com

Mwaka jana serikali iliamua kuleta utaratibu mpya wa upatikanaji wa
pembejeo kwa mkulima, ambao unategemewa kuanza msimu huu. Utaratibu
huu ni wa "mkopo wa pembejeo kwa mkulima" kupitia vikundi hasa AMCOS
na SACCOS. Utalenga hasa kwenye zao la mahindi ili kuzalisha chakula
cha kutosha. Pesa hiyo itajizungusha yenyewe kila mwaka.
Ni mpango mzuri sana ambao kama utasimamiwa vizuri utamkomboa
mkulima mdogo mdogo ambaye hasa ndiye mwenye kuchukua changamoto
nyingi za kilimo. Utaratibu huu uko hivi: Mkulima anatakiwa atoe 20%
ya pembejeo anazohitaji kama hisa kwenye kikundi au ushirika. Serikali
itamkopesha 80% iliyobaki. Baada ya kuvuna mkulima atatakiwa apeleke
mazao yake ghalani, masoko yatatafutwa na mkulima atalipa deni kwa
serikali kwa riba isiyozidi 5% na mkulima huyu atabaki na salio
lililobaki. Ni mpango mzuri sana. Utamnufaisha sana mkulima.
Lakini sasa changamoto zipo nyingi sana kwenye mpango huu kama vile:

1. Upatikanaji wa pembejeo kwa wakati kwa mkulima-Je, mbegu na mbolea
zitamfikia mkulima kwa wakati? au zitafika mwezi january! Hii inaihusu
serikali kuwahi kutoa 80% ili mawakala waweze kusambaza kwa wakati.

2. Urejeshaji wa mkopo- Hii inamhusu mkulima, utashi wake katika hili.
Mkulima atachukua mbegu na mbolea, atalima, Je, atapeleka ghalani? Na
pia kama hautakuwepo usimamizi dhabiti, wapo watakaochukua na
asizipeleke shambani, anauza.

3. Pembejeo kutosheleza mahitaji kwa wakati- Je, serikali itatoa kwa
wakati mmoja mahitaji ya wakulima wote? Kwa mfano katika kijiji changu
20% ni 5.4milioni, zitakuja zote kwa pamoja? Labda katika hili
ningetoa ushauri kwamba wangepiga mahesabu ya kiasi cha mbegu na
mbolea ya kupandia ndizo ziwahi mapema, kisha wale mbolea ya kukuzia
endapo pesa ya mkupuo haipo.

Hizo changamoto tatu zinatakiwa kuangaliwa sana, maana zinaweza
kukwamisha mpango mzima.
Mpaka sasa hazijaanza kusambazwa, lakini ni matumaini yangu kuwa
zitawahi mapema mwezi huu wa November.
Ahsanteni sana na karibuni kwa michango na maoni yenu katika hili.

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete