Wednesday, November 20, 2013

(i) MATANGO

Asili yake ni Afrika au Asia, lakini kwa sasa hustawishwa katika sehemu nyingi za kitropiki. Matunda yake hukatwa katwa na kuliwa kama achali, au kachumbali, au huwekwa kwenye siki, au hupikwa na kuliwa.

Kuna aina nyingi, lakini hutofautiana kwa umbo na rangi. Aina zinazojulika zaidi hapa kwetu ni: Colorad, Telegraph, Palmetto, Chicago, Pickling, Straight 8 na Marketer.

Ustawishaji: Zao hili huhitaji hali ya joto na hukua kwa haraka sana. Hustawi katika aina nyingi za udongo. Hatua za kupanda mbegu ni sentimeta 60 hadi 75 kati ya mimea, na hatua hizo hizo kati ya mistari. Mimea michanga inatakiwa iwekewe kinga ili isidhuriwe na upepo.
Matango hukua na kukomaa kwa haraka zaidi katika udongo mwepesi, lakini hutoa mavuno makubwa zaidi katika ardhi nzito kiasi. Hata hivyo ardhi inayotuamisha maji haifai, na ikibidi mimea ipandwe kwenye matuta.
Zao hili hutumia chakula kingi kutoka ardhini, kwa hiyo ni muhimu kuweka samadi au mbolea ya takataka mara kwa mara. Matunda huwa tayari kuvunwa baada ya majuma sita hadi manane tangu kupandwa.

Magonjwa: (a) Bacteria Wilt- Majani yaliyoshambuliwa hunyong'onyea na kudhoofu na hatimaye hufa. Mmea ukikatwa huchuruzika ute mzito. Nyunyizia dawa ya Copper kila baada ya siku 10 na tumia aina zenye uvumilivu mkubwa kama vile Palmetto.

(b)Powdery Mildew- Ukungu wake hushambulia majani na mashina. Nyunyizia dawa ya unga ya sulphur kila baada ya siku 10.

(c)Cucumber Mosaic- Husababishwa na sumu (virus). Hali ikiwa mbaya zaidi mmea hugeuka njano, hudumaa na hushindwa kutoa matunda. Huenezwa na magugu au wadudu kama aphids na beetles. Usafi bustanini unahitajika.

Wadudu: (a)Cucumber Beetle- Huyu ni mdudu mbaya sana kwa zao hili. Hutafuna miche ya matango na maboga mara ichipuapo, pia hushambulia majani ya mimea michanga.

(b)Melon Aphid- Hufyonza utomvu wa mimea. Tumia Malathion,Nicotine. Hakisha dawa inafikia upande wa chini wa majani

(c)Pickle Worm- Buu au funza hujipenyeza ndani ya ua,kisha huhamia kwenye tunda.Tumia Rotenone au Crylite kila baada ya juma 1.��hina.

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete