Thursday, January 2, 2014

Ndigana baridi (Anaplasmosis) ni ugonjwa unaosababishwa na kupe, mbung'o na inzi aina ya Stomoxys kwa mifugo yako hasa ng'ombe, mbuzi na kondoo.

JINSI UGONJWA HUU UNAVYOAMBUKIZWA (Mode of transmission of the disease)

Ugonjwa wa ndigana baridi unaambukizwa kupitia kwenye ng'ombe mgonjwa baada ya kuumwa na kupe, mbung'o au inzi, aina ya ng'ombe, mbuzi au kondoo walio na afya nzuri ili kupata chakula yaani kunyonya damu wakati wananyonya damu pia ng'ombe asiye mgonjwa. Pia kwa njia ya kutumia vifaa vya kitaalamu ambavyo havikuchemshwa sawasawa kama sindano, vijidudu vya ugonjwa husambazwa kutoka mnyama mgonjwa kwenda mnyama mwenye afya kwa kutumia vifaa hivyo.

Hivyo uangalizi mkubwa unatakiwa wakati shughuli hizo za kuchoma sindano, kukata pembe n.k. zinapofanyika.

WANYAMA WANAOPATA UGONJWA WA NDIGANA BARIDI.
- Ng'ombe
- Mbuzi
- Kondoo

Ndama wadogo hawapatwi na ugonjwa huu.

DALILI KUU ZA UGONJWA.

Dalili kuu za ugonjwa huu ni:-
(i) Homa kali (40-41C).
(ii) Kinyesi kigumu sana na chenye utando mweupe juu yake.
(iii) Kupumua/kuhema kwa shida.
(iv) Mnyama kushindwa kucheua.
(v) Rangi ya njano mdomoni, puani na sehemu zilizo wazi za mnyama kama machoni n.k.
(vi) Kukosa hamu ya kula.
(vii) Kupunguza uzalishaji wa maziwa.
(viii) Kutokunywa kwa sababu ya omasum kutofanya kazi (constipation).

MAGONJWA MENGINE YANAYOFANANA NA NDIGANA BARIDI.

-Ndigana kali
-Kuvimbiwa (bloat)
-Kichomi

JINSI YA KUZUIA UGONJWA WA NDIGANA KALI.

-Hakikisha wanyama wako wanaogeshwa vizuri na dawa ya kuua kupe (Acarcides)
-Ogesha kwa kutumia dawa zinazozuia kupe na mbung'o mara 1 kwa wiki mfano Tristix, Tixfix, Ciberdip, Paranex, Alfanex, Steladone, Dominex n.k.
-Chunga mifugo yako katika mbuga zisizo na kupe au mbung'o.
-Ikiwezekana chunga/lisha kwa mzunguko (rotational grazing) katika mbuga zako ili kupunguza kuzaliana kwa kupe.

JINSI YA KUTIBU MNYAMA MWENYE NDIGANA BARIDI

-Watibiwe kwa kutumia dawa ya Oxytetracycline ya sindano 5-10mg/kg ya uzito
-Wanyama waliofunga choo wanyweshwe mafuta ya kupikia ili kulainisha tumbo

Ahsanteni!��igana

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete