Tuesday, December 10, 2013

  Mboga za majani zinashika nafasi muhimu sana katika vyakula vyetu.
 Zinaliwa kila na mara nyingi zaidi ya mara moja kwa siku. Zipo aina nyingi za mboga za majani , zingine zinalimwa na zingine zinaota zenyewe porini na mashambani wakati wa msimu wa mvua. Mboga zina virutubisho kama madini na vitamini ambavyo vinahitajika mwilini kwa afya bora. Hata hivyo pamoja na kwamba vina virutubisho vya kutosha, na zinaliwa kila siku, watu wengi wanapata matatizo ya afya yanayotokana na ukosefu wa virutubishi vinanyotokana katika mboga za majani kwa mfano upofu na upungufu wa damu.

Hali hii inajitokeza kwa sababu gani?

  Mojawapo ya sababu ya kuvikosa virutubishi ni utayarishaji usiokuwa mzuri wa mboga za majani kabla ya kula. Utayarishaji wa mboga hizi ni shughuli zote zinazohusiana na kuandaa, kupika na kuweka tayari kwa kula. Wakati wa utayarishaji virutubishi muhimu vinaweza kupotea kama mambo muhimu hayazingatiwi. Kupika ni muhimu kwa sababu kuna faida zifuatazo;

             FAIDA ZA KUPIKA

- Kupika kunaua vijidudu vibaya viletavyo magonjwa kwenye chakula.
- Kunaua vimeng'enyo vilivyomo ndani ya chakula ambavyo vinaweza kuharibu chakula.
- Kubadili rangi na kuboresha radha ya chakula.
- Kuboresha uyeyushaji wa chakula mwilini.

  Pamoja na faida hizi, kupika chakula pia kunaweza kuleta upotevu wa virutubishi muhimu iwapo hautafanyika vizuri.

            DOSARI ZA UTAYARISHAJI

- Mboga nyingi huchambuliwa na kukatwakatwa vipande vidogo ndipo zinaoshwa.
- Mboga hubandikwa jikoni na maji baridi.
- Baadhi ya mboga huchemshwa na maji mengi halafu maji yanayochemshia humwagwa.
- Kama mboga ni kavu zinalowekwa kwenye maji halafuayale maji yanamwagwa.
- Mboga inapikwa kwa muda mrefu sana zaida ya nusu saa na mara nyingine bila kufunikwa.
- Mara nyingine mboga haziliwi mara tu baada ya kutayarishwa.

            KWA NINI UTAYARISHAJI WA NAMNA HII HAUFAI.

  Upishi wa namna hii unasababisha upotevu wa virutubisho muhimu kama vitamini C, A na vitamini B1, vitamini hizi muhimu zinayeyuka kwenye maji kwa urahisi, kwa unapokatakata vipande vidogo vidogo na kuosha kwa kiasi kikubwa zinapotea kwenye maji uliyotumia kuoshea au kupikia iwapo maji hayo yanamwagwa na hivyo virutubisho hivi muhimu hupotea. Mboga zioshwe kwanza kabla ya kukatakata.

           VITAMINI C HUPOTEA PIA IKIWA;

- Mboga zinatayarishwa halafu zinaachwa kwa muda mrefu kabla ya kupikwa.
- Mboga zinapikwa na kuachwa kwa muda mrefu kabla ya kuliwa.
- Mboga zinapoa halafu zinapashwa moto kabla ya kuliwa.

            VITAMINI A HUPOTEA WAKATI WA KUTAYARISHA MBOGA KAMA;

- Mboga inachemshwa kwa muda mrefu bila kufunikwa.
- Mboga inakaangwa kwenye mafuta yenye joto kali kwa muda mrefu.

             MADINI MUHIMU HUPOTEA IKIWA;

- Maji yanayochemshia mboga humwagwa.

      Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa utayarishaji wa mboga za majani.

- Chagua mboga nzuri ambazo hazijasinyaa au kuanza kuoza.
- Zingatia usafi wakati wa kupika kama ifuatavyo;
                   * Tumia maji safi
                   * Mahali pa kupikia pawe safi
                   * Vyombo vyote vinavyotumika viwe safi
                   * Nawa mikono na sabuni kabla ya kuanza kupika na uwe msafi
- Osha mboga kwa maji safi kabla ya kukatakata
- Loweka mboga kavu kwenye maji ya kutosha tu kuzifunika na tumia maji hayo wakati wa kupika mboga hiyo.
-Kama mboga ni za kuchemsha, chemsha mboga kwenye maji kidogo yanayochemka ya kutosha kuivisha mboga. Usimwage maji ambayo umetumia kuchemshia mboga.
- Pika mboga za majani kwa muda mfupi iwezekanavyo, na isizidi robo saa kutegemeana na aina ya mboga mboga.
- Kula au tumia mboga mara baada ya kupika. Hivyo unapaswa kupika mboga yako muda mfupi kabla ya kula.
- Mboga za majani zisiachwe kwenye hali ya uvuguvugu kwa muda mrefu kwani virutubishi vingi hupotea zaidi katika hali hiyo.

Ahsanteni sana na maandalizi mema ya mapishi.
 

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete