Monday, September 26, 2016

Leo nataka nikuonyeshe jinsi ya kutengeneza chakula cha vifaranga wadogo yaani wa wiki 1 hadi wiki 4.

Mahitaji muhimu katika utengenezaji wa chakula cha vifaranga kilo 100.

Pumba ya mahindi 40kg,

Mahindi ya kuparaza 10kg,

Mashudu ya alizeti 20kg,

Dagaa 24kg,

Unga wa mifupa 5 kg,

Chokaa 1/4kg,

Chumvi iliyo sagwa 1/2kg

Chikpremix 1/4kg.

Hayo ndio mahitaji muhimu katika uandaaji wa chakula cha vifaranga kilo 100.
Ndugu kumbuka kuwa unaweza kutengeneza chakula hicho kwa ajili ya vifaranga wako na pia unaweza pia ukafanya biashara ya kuuza chakula cha kuku kwa kuanza na hicho cha vifaranga wadogo, jua kuwa katika jamii sio kila mfugaji anaweza kutengeneza chakula cha kuku kuna wengine wanaweza lakini hawana mda wakutengeneza na pia kuna wengine hawajui kabisa jinsi ya kutengeneza, Ndugu msomaji wa mtandao huu ningependa utajirike na ufugaji kwa kuanzia na biashara ya uuzaji wa vyakula vya kuku. Leo anza kutengeneza hicho kwa kilo 100 unaweza kutengeneza ata kg 200kg, 300kg, 500kg ata 1000kg cha kufanya wewe ndiye unapaswa kuongeza mahitaji kwa kadri uwezavyo .

Prepared by:

Marcodenis E. Misungwi

Agriculture Extensionist.

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete