Sunday, April 13, 2014

Jopo la waheshimiwa madiwani, Kamati ya Uchumi wametembelea mradi wa maji kwa ajili ya huduma za umwagiliaji katika kijiji cha Nansama kata ya Isansa.

Mradi huu ulianzishwa kwa uwezeshwaji kama kikundi cha kahawa Igabda na benki ya NMB chini ya kitengo chao cha Development Foundation ukigharimu Tsh. 30,000,000/= hata hivyo baada ya ujenzi kumalizika na watu kuanza kutumia, lilibomoka na halmashauri kupitia Idara ya Kilimo iligharamia ukarabati huo. Na tokea hapo mradi sasa uko chini ya halmashauri.

Kamati iliongozana na jopo la watumishi kutoka katika Idara mbalimbali hasa zinazoshabihiana na Kilimo wakiongozana na Mkaguzi wa ndani.

Kamati ilimuomba mwenyekiti wa bwawa atoe maelezo ni historia fupi juu ya jinsi mradi ulivyoanzishwa na unufaika wa wananchi katika mradi huo. Mwenyekiti alieleza kwa kifupi na kukumbushia ushauri uliokwishatolewa na mkuu wa mkoa pindi alipotembelea mradi h mwezi January wa halmashauri kuweza kuangalia uwezekano wa kulipanua zaidi ambapo sambambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa alishauri miti ipandwe kulizunguka bwawa ambalo hilo l miti limekwisha tekelezwa na miti imepandwa na inaendelea vizuri. Maswali mawili matatu pamoja na ushauri yakaulizwa.

Bi. Lydia Shonyela, ambaye alimwakilisha Afisa Kilimo na Umwagiliaji (DAICO) pia alitoa baadhi ya maelezo ya jinsi halmashauri ilivyosaidia katika mradi huo.

Baada ya hapo waliondoka kuelekea kata Ruanda.

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete