Sunday, April 27, 2014

Uzoefu umeonyesha kuwa wafugaji wengi wa kuku wa kisasa (Commercial Chicken). Kuku hupatwa na magonjwa ya virusi licha ya kuwa wamechanjwa. Tatizo hili limekuwa likitokea hasa kwa ugonjwa Gumboro (Infectious Bursal Disease).

Zipo sababu ambazo kama mfugaji hakuzingatia kanuni na taratibu za uchanjaji kuku ugonjwa unaweza kutokea.

. Ratiba ya chanjo.

Kutokufuata ratiba ya utoaji chanjo (Vaccination Programme) iliyopendekezwa na mtaalam wa mifugo wa eneo au kanda husika, kunaweza kusababisha kuku wasipate uwezo wa kujikinga na ugonjwa huo ingawa watakuwa wamechanjwa. Hivyo inashauriwa kufuata ratiba ya utoaji wa chanjo iliyopendekezwa kitaalam.

. Utunzaji mbaya wa Chanjo.

Chanjo iliyohifadhiwa katika joto kali hupoteza uwezo wa kufanya kazi. Vile vile kuweka Chanjo kwenye freezer huathiri uwezo wa Chanjo husika.
Inashauriwa Chanjo kuhifadhiwa kwenye hali ya ubaridi wa joto kati ya nyuzi joto 2°C-8°C hasa kwenye friji.

Kumbuka kwamba kuna baadhi ya chanjo kwa sasa zimepigwa marufuku kusambazwa kwa kuonekana kuchakachuliwa na kupoteza ubora wake wa kutibu. Chanjo iliyozuiwa ni ya "Matone" inayozuia ugonjwa wa Kideri. Ni vema ndugu mfugaji uwe mfuatiliaji wa mambo kila wakati.

. Ugonjwa

Iwapo kuku tayari wameshapata virusi vya ugonjwa husika, wanaweza wakaugua ugonjwa huo hata kama watachanjwa chanjo ya ugonjwa huo.

Kwa hiyo basi kabla hujawachanja kuku wako wachunguze kwanza kama hawana dalili ya kuugua, lakini la muhimu kuliko yote ni kuzingatia ratiba ya uchanjaji maana yawezekana wakawa hawaonyeshi dalili ya kuugua lakini kumbe wadudu wakawa wameshaingia.

. Kutofuata masharti ya watengenezaji wa Chanjo kuhusu matumizi ya Chanjo.

Mbali na maelekezo ya matumizi ya chanjo ambayo hutolewa na wataalamu wa mifugo au wauza madawa ya mifugo wanaotambulika katika kutoa huduma hiyo. Ni muhimu pia kuzingatia masharti ya mtengenezaji chanjo husika.

. Usafirishaji na utoaji Chanjo.

Usafirishaji wa chanjo katika mazingira yasiyofaa huathiri nguvu ya Chanjo, pia utoaji wa Chanjo yenyewe na wataalam wa mifugo au madawa ya mifugo huathiri zoezi lote (Vaccination Procedure) la uchanjaji wa kuku. Inaahauriwa Chanjo isafirishwe kwenye chombo au kifaa chenye ubaridi au chenye uwezo wa kuhifadhi joto linalotakiwa, pia kuzingatia taratibu zote za mwenendo wa kuchanja kuku.

. Lishe duni.

Chakula ambacho kina viinilishe duni vinavyohitajika kukidhi afya bora ya kuku husababisha kuku kuwa dhaifu, hivyo huwa mwili wa kuku hauna uwezo wa kujikinga na magonjwa. Hivyo ni vema kulisha chakula cha kuku chenye ubora unaokidhi mahitaji ya afya ya kuku.

. Utumiaji wa dawa za tiba na chanjo kwa pamoja.

Hii pia huathiri uwezo wa Chanjo kufanya kazi kwenye mwili wa kuku. Ni vema kutowapa chanjo na dawa za tiba (antibiotics) kwa wakati mmoja. Inashauriwa kutowatibu kuku siku mbili kabla na baada ya chanjo kutolewa pia wapewe vitamini kama Vitalyte, Poultry antistress, Vitastress, Stressvita n.k.

. Vijisumu (mycotoxins).

Hivi ni vijisumu ambavyo huwa kwenye chakula cha kuku kilichohifadhiwa vibaya kama vile unyevunyevu au kwenye tandiko chafu, hivyo kuku akila chakula chenye vijisumu hivi hupunguza kinga za mwili kupambana na magonjwa, kwani vijisumu hivi hushambulia sehemu muhimu ndabi ya mwili wa kuku ambazo hujihusisha na kinga na magonjwa. Hivyo inashauriwa vyakula vya kuku vihifadhiwe kwenye sehemu isiyokuwa na unyevunyevu au joto kali, pia nafaka zinazotumika kutengeneza chakula cha kuku changanya na vitu vinavyosaudia kupambana na vijisumu hivi. Waweza kutumia Farmacid premix na mycobind kwenye chakula.

. Usumbufu (Stress)

Kuku waliopata usunbufu siku chache kabla au baada ya chanjo huwa wanapungukiwa na uwezo wa kupokea chanjo ili kujikinga na ugonjwa, usumbufu unaweza kuwa msongamano (overstocking), kukata midomo (beak trimming), kuwahamisha kuku kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Hivyo epuka usumbufu kwa kuku unapokaribia muda wa kuwapa Chanjo ili kufanya chanjo ifanye kazi vizuri.

Imetayarishwa na Marcodenis E. Misungwi, Mtaalam wa Kilimo na Mifugo.

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete