Thursday, February 27, 2014

Ili kufanikiwa katika kilimo kunahitajika Pembejeo bora mashambani. Pembejeo hizo zinahitaji fedha, na wakulima wetu wengi ni wakulima wadogo wadogo (smallholders farmers) ambao kila mwaka wanadunduliza hapa na pale kujitafutia pembejeo na mara nyingi hazitoshelezi kumudu mashamba yao.

Kwa kuliona hilo, watafiti (Researchers) kutoka katika kituo cha utafiti Uyole (ARI-Uyole) chini ya Mtafiti William Mmari wameweza kuja na mradi ambao unadhaminiwa (funded) na Agriculture Green Revolution for Africa, AGRA, chini ya mwenyekiti wake Koffii Annan. Mradi huu unafanya mambo mengi kwa mkulima huyu mdogo mdogo na kati ya mambo hayo ni "Mikopo ya Pembejeo kwa Wakulima". Mkulima anakopeshwa pembejeo ya kutosha kuhudumi ekari moja ama ya Mahindi au Maharage, kisha atarejesha mkopo huo wakati wa mavuno na riba kidogo ya uendeshaji ambayo si kubwa ya kumuumiza mkulima.

Katika kuongeza ufanisi wa mradi huo wa mikopo ya pembejeo kwa wakulima, ARI-Uyole wamewaita kuwapa mafunzo wataalam wa kilimo (Extension Officers) wa kata na vijiji vinavyoguswa na mradi kutoka katika wilaya za Mbozi na Mbeya vijijini. Mafunzo hayo yalichukua siku mbili yakilenga hasa kuzijua mbinu njia ambazo mkulima huyu aliyekopeshwa pembejeo aweze kuzalisha vizuri na kurudisha mkopo wote na yeye kubakiwa na ziada.

Washiriki walijifunza kwamba, ili mkulima aweze kuhudumia shamba vizuri, ni lazima ajiwekee akiba ambayo itamsaidia katika manunuzi ya pembejeo wakati wa kulima. Mkulima ashauriwe kujiunga na vikundi vya wakulima vya kuweka na kukopa kama, AMCOS, ambavyo kwa sasa vimesamba sana huko vijijini na wamiliki ni wakulima wenyewe.

Katika hali ya kawaida uzoefu unaonyesha kwamba, watu wengi wana fikra ya msaada (kusaidiwa) katika akili zao. Hili linadhoofisha sana Mikopo hasa hii ya Pembejeo. Ili kudhibiti hilo Mikopo ya Pembejeo ya AGRA inapitia kwa wanachama hai kwenye AMCOS na wataunda vikundi vidogo ndani mwao ili waweze kujisimamia.

Matarajio ya Mradi ni kumjengea uwezo mkulima ili aweze kujiendeleza mwenyewe na apanue kilimo chake.

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete