Tuesday, February 18, 2014

Zao hili nalo pia ni geni katika nchi hii, lakini kwa kuwa linaendelea kulimwa na hupendwa na wakazi wengi, ni vizuri kuelewa jinsi ya kulistawisha.

Igawa zao lilistawishwa tangu zama za Warumi, ni katika karne hii tu ambapo limeenezwa na kutumiwa katika sehemu nyingi duniani. Kwa sasa mboga hii hustawishwa sana katika nchi nyingi za tropiki, hasa Afrika na Visiwa vya Caribbean.

Brokoli ina kiasi kikubwa cha Vitamini A. Sehemu inayotumiwa ni kichwa au ua la mmea ambalo kidogo hufanana na koliflawa. Tofauti kubwa ni kwamba tunda lake ni mkusanyiko wa vichwa au ni shada la maua madogo madogo yaliyokusanyika pamoja bila ya kubanana sana. Rangi ya matunda ni kijivu-kijani, au kibluu-kijani, au kijani iliyofifia. Brokoli huchukua muda mrefu zaidi kukua na kukomaa kuliko kabeji.

AINA: Kama yalivyo mazao mengine, pia kuna aina kadhaa za zao hili ambazo hupendelewa zaidi na wakulima au walaji, kwa mfano Calabrese, De Cicco, Texas 107, Carvet Hybrid, Barca Hybrid, Green Sprouting na Mountain.

Wakati wa kuvuna, ua lote hukatwa pamoja na sehemu ya juu ya shina ambayo ni laini. Vile vile unaweza kuongeza kidogo cha majani yazungukayo ua. Mapishi na matumizi yake ni sawa na ya kabeji au koliflawa; yaani huchemshwa na kutengenezewa mchuzi, au kufanywa supu na rojorojo.

USTAWISHAJI: Brokoli huweza kustawi katika sehemu ambazo koliflawa hustawi, lakini ina uwezo mkubwa zaidi wa kuvumilia joto na uhaba wa mvua. Ili kupata matunda makubwa, ni muhimu kuhakikisha kwamba matunda hayo yanavunwa nyakati za baridi. Hii ni kwa kuwa hali ya joto husababisha matunda kukua kwa haraka mno kiasi kwamba ni vigumu kufuata utaratibu wa kuyavuna kidogo kidogo na kwa wakati unaostahili. Hakikisha udongo hautepeti na kutuamisha maji. Unaweza kuongeza mavuno kwa kuweka mbolea ya Nitrogen (Sulphate of Ammonia).

MAGONJWA: Magonjwa na wadudu washambuliao zao hili ni sawa na wa kabeji na koliflawa.

KUVUNA: Kwenye sehemu za joto tunda la kwanza huvunwa siku 60-70 tangu kupandikizwa. Na kwa nyanda za juu, siku 100-120.

Ahsanteni!

1 comments:

  1. CONTACT: onlineghosthacker247 @gmail. com
    -Find Out If Your Husband/Wife or Boyfriend/Girlfriend Is Cheating On You
    -Let them Help You Hack Any Website Or Database
    -Hack Into Any University Portal; To Change Your Grades Or Upgrade Any Personal Information/Examination Questions
    -Hack Email; Mobile Phones; Whatsapp; Text Messages; Call Logs; Facebook And Other Social Media Accounts
    -And All Related Services
    - let them help you in recovery any lost fund scam from you
    onlineghosthacker Will Get The Job Done For You
    onlineghosthacker247 @gmail. com
    TESTED AND TRUSTED!

    ReplyDelete