Wednesday, October 19, 2016

UFUGAJI BORA WA NG'OMBE WA MAZIWA.

Ng'ombe hutoa maziwa lakini pia hutoa mazao mengine kama ngozi,mbolea na hutumika kama wanyama kazi. Zaidi ya asilimia 95 ya ng,ombe hutumika kama wanyama kazi.

Zaidi ya asilimia 95 ya ng’ombe wanaofugwa hapa nchini ni wa asili ambao huzalisha nyama na maziwa kwa kiwango kidogo ikilinganishwa na wale wachache walioboreshwa. Ng’ombe walioboreshwa wamegawanyika katika makundi mawili.
.Wale wanaofugwa kwa ajili ya nyama na wanaofugwa kwa ajili ya maziwa.

Ili kuwawezesha ng’ombe kuzalisha mazao bora ya nyama, maziwa na ngozi mfugaji anapaswa kufuata kanuni za ufugaji bora ambazo ni pamoja na:-

Kufuga ng’ombe katika eneo kwa kuzingatia uwiano wa idadi ya ng’ombe na malisho katika mfumo wa ufugaji huria.
1. Kujenga banda au zizi bora.

2. Kuchagua koo/aina ya ng’ombe kulingana na uzalishaji (nyama au maziwa).

3.Kutunza makundi mbalimbali ya ng’ombe kulinga na umri na hatua ya uzalishaji.

4. Kumpa ng’ombe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili.

5. Kudhibiti magonjwa ya ng’ombe kama inavyoshauriwa na mtaalamu wa mifguo.

6. Kuvuna mifugo katika umri na uzito muafaka kulingana na mahitaji ya soko.

7. Kuzalisha maziwa, nyama na ngozi zinazokidhi viwango vya ubora na usalama.

8. Kutunza kumbukumbu za uzalishaji na matukio muhimu ya ufugaji.

MIFUMO YA UFUGAJI.

Ng’ombe wanaweza kufugwa katika mfumo wa ufugaji huria au kulishwa katika banda (ufugaji shadidi).

Ufugaji huria huhitaji eneo kubwa la ardhi yenye malisho mazuri na vyanzo vya maji. Pamoja na kuwa na ufugaji huu, ni muhimu ardhi hiyo itunzwe kwa kuzingatia uwiano wa idadi ya ng’ombe na malisho. Ufugaji wa shadidi uzingatie uwepo wa banda bora na lishe sahihi.

UFUGAJI KATIKA MFUMO HURIA.

Ili mfugaji aweze kupata mazao mengi na bora katika ufugaji huria anapaswa kuzingatia yafuatayo:-

1. Atenge eneo la kutosha la kufugia kulingana na idadi ya ng’ombe alionao.

2. Atunze malisho ili yawe endelevu na yapatikana wakati wote.

3. Awe na eneo lenye maji ya kutosha na Atenganishe madume na majike ili kuzuia ng’ombe kuzaa bila mpangilio.

Matunzo mengine ya ng’ombe yazingatie vigezo vingine muhimu kama;
   - umri,
    - hatua ya uzalishaji
     - matumizi ya ng’ombe      husika.

BANDA/ZIZI BORA LA NG’OMBE BANDA BORA.

Banda lijengwe sehemu ya mwinuko mbali kidogo na makazi ya watu na liwe na sifa zifuatazo; 

1. Uwezo wa kumkinga ng’ombe dhidi ya mvua, upepo, jua kali na baridi.

2. Kuta imara zenye matunda au madirisha kwa ajili ya kuingiza hewa na mwanga wa kutosha, Sakafu yenye mwinuko upande mmoja ili isiruhusu maji na uchafu kutuama.

3. Lijengwe katika hali ya kuruhusu kufanyiwa usafi kwa urahisi kila siku, na sakafu ngumu ya zege au udongo ulioshindiliwa na kuweka malalo.

4. Paa lisilovuja.

Aidha kwa wafugaji wanaofuga katika ufugaji huria ambako mazizi hutumika, inashauriwa kuzingatia yafuatayo:-

1.Zizi likae mahali pa mwinuko pasiporuhusu maji kutuama.

2. Zizi liweze kukinga mifugo dhidi ya wezi na wanyama hatari.

2. Ukubwa wa zizi uzingatie idadi na umri wa mifugo ng’ombe watengwe kulingana na umri wao.

3. Zizi lifanyiwe usafi mara kwa mara na Liwe na sehemu ya kukamulia (kwa ng’ombe wa maziwa), stoo ya vyakula, sehemu ya kutolea huduma za kinga na tiba, eneo la kulishia na maji ya kunywa.

ZIZI BORA.

Zizi lijengwe sehemu ya mwinuko isiyoruhusu maji kutuama mbali kidogo na makazi ya watu na liwe na sifa zifuatazo:-

1.Liweze kuhakikisha usalama wa ng’ombe. Ukubwa wa zizi uzingatie idadi ya mifugo.

2. Liwe na sakafu ya udongo ulioshindiliwa vizuri na kufanyiwa usafi mara kwa mara.

3. Zizi la ndama liwe na paa ma Lijengwe kwa vifaa madhubuti na visivyoharibu ngozi.

KUMBUKUMBU NA TAKWIMU MUHIMU.

Kumbukumbu ni taarifa au maelezo sahihi yaliyoandikwa kuhusu matukio muhimu ya kila ng’ombe na shughuli zote zinazohusiana na ufugaji. Mfugaji anashauriwa kuweka kumbukumbu na takwimu muhimu katika shughuli zake za ufugaji wa ng’ombe. Kumbukumbu zinamsaidia mfugaji kujua mapato na matumizi na kufanya maamuzi sahihi kuhusu mifugo husika na mazao yake. Aidha humwezesha kuweka mipango ya shughuli zake. Mfugaji anapaswa kuweka kumbukumbu muhimu zifuatazo:-

1. Uzazi (uhamilishaji na matumizi ya dume, tarehe ya kupandwa, kuzaa na kuachisha kunyonya)

2. Kinga na tiba

3. Utoaji wa maziwa

4. Ukuaji

5. Idadi ya ng’ombe kwa makundi – majike, ndama, mitamba, madume,maksai.

Ahsanteni

Prepared by:

Marcodenis E. Misungwi

Agriculture Field Extensionist.

Tuesday, October 18, 2016

KILIMO BORA CHA MAHINDI

Mahindi ni zao linalolimwa katika maeneo mengi hapa nchini, linahimili katika udongo wenye uchachu wa 6-6.5. Hustawi zaidi kwenye maeneo yenye mwinuko wa 2500. Zao la mahindi kama mazao mengine lina kanuni Zake.

KANUNI YA KWANZA: KUTAYARISHA SHAMBA MAPEMA.

Tayarisha shamba la mahindi mara tu baada ya kuvuna mazao ya msimu uliopita. Mahindi hustawi sehemu yenye udongo wenye rutuba na usiosimamisha maji. Moto usitumike Kuandaa shamba.

FAIDA ZA KUTAYARISHA SHAMBA MAPEMA.

Baada ya kuvuna,udongo bado ni mlaini hivyo hulimika kwa urahisi kwa kutumia jembe lolote. Masalia yatakayofunikwa udongoni huoza mapema. Hupunguza magugu. Hupunguza wadudu waharibifu.

KANUNI YA PILI: KUPANDA.

Wakati wa kupanda hutatanisha kwani mvua hayatabiriki,Kama mvua hunyesha nyakati na majira yale yale ya mwaka basi kalenda ifuatayo inaonyesha tahere za kupanda zao la mahindi katika eneo lako. Mbeya na maeneo ya jirani, mwanzoni mwa mwezi Novemba hadi Desemba mwishoni. Morogoro na maeneo ya jirani, Mwezi Januari katikati hadi Februari katikati Iringa na maeneo ya jirani, katikati ya mwezi Novemba hadi Desemba mwishoni Songea na maeneo ya jirani, katikati ya mwezi Novemba hadi Januari mwanzoni. Kupanda mahindi mapema ni muhimu kwani uwezekano wa kuvuna mazao mengi ni mkubwa. Kwa mashamba makubwa makubwa sana wakati wa kupanda uwe wiki moja kabla ya mvua kuanza kunyesha na isizidi wiki mbili kabla ya mvua. Isiwe mapema zaidi kwani mbegu zitaharibiwa na joto kati ya udongoni wadudu,panya,ndege na wanyama wengineo.

FAIDA ZA KUPANDA MAPEMA.

Mahindi yanapata mvua ya kutosha hadi kukomaa. Magonjwa kama yale ya ya majani (streak ugonjwa wa milia) hayatatokea au yatakuwa kidogo. Mbolea uliyoweka itayeyuka pamoja na mahindi yastawi vizuri.

KANUNI YA TATU: KUCHAGUA MBEGU BORA.

Mbegu bora ni zile zilizo zalishwa kitaalamu. Ni safi hazijabunguliwa na wadudu. Huzaa mazao mengi. Hustahimili magonjwa.

AINA ZA MBEGU.

1. Mbegu aina ya chotara (hybrid).
2. Aina ya ndugu moja(synthetic).
3. Mbegu aina ya composite.

Mbegu za kisasa zikitumiwa vizuri katika misingi ya kilimo, zina uwezo wa kuzaa magunia 50-80 au tani 5.5 – 7.5 kwa hekta moja au gunia 20-35 kwa hekari.

MAPENDEKEZO YA MBEGUZA KUPANDA.

Kuna mbegu nyingi za kisasa zilizoko kwenye soko mfano SIDCO ,PANNAR, PIONEER, KITALE kutoka KENYA n.k.
Ni vyema kufuata ushauriwa wataalamu wa kilimo.

KANUNI YA NNE KUPANDA.

Idadi ya mimea katika eneo ni muhimu kwani uzoefu unaonyesha wakulima wengi hawapati kiwango kinachotakiwa kutokana na upungufu wa idadi ya miche katika eneo husika. Na athari zake ni:-
1. Mazao hupungua.
2. Mmea huangushwa na upepo Mabua mengi hayazai. 3. Idadi ya mimea nayo ikipungua kwenya eneo husababisha mavuno kupungua jambo la kufanya ni kupanda mbegu katika nafasi sahihi zilizoshauriwa na wataalamu na kupanda kwa wakati na kwa umakini.

KIASI CHA KUPANDA.

Mbegu za mahindi huhifadhiwa kwa dawa kali na kiasi cha 10kg hutosha kupanda ekari moja. Nafasi za kupanda. 75cm x 30cm mche mmoja 75cm x 60cm miche miwili 90cm x 45cm miche miwili

KANUNI YA TANO; KUTUMIA MBOLEA.

Mahindi hustawi na kuzaa vizuri iwapo yatapatiwa mbolea pamoja na matunzo mengine ya kilimo bora. Ukipanda mbegu bora bila kutumia mbolea ni kazi bure.

KUNA AINA KUU MBILI ZA MBOLEA.

1. Mbolea za asili mfano; samadi,mboji na majani mabichi,mbolea hizi hazina virutubisho vya kutosha.
2. Mbolea za viwandani; ambazo hizi zimegawanyika katika makundi mawili ambayo ni za Kupandia na za kukuzia.

KANUNI YA SITA: KUVUNA KWA WAKATI.

Ili kuhakikisha upatikanaji wa kipato cha kutosha, ni lazima kuhakikisha kuwa mahindi yanavunwa kwa wakati. Utafiti unaonyesha kuwa 30% ya mavuno hupotea katika mchakato wa uvunaji, usafirishaji mpaka sokoni. Kwa ni muhimu sana kufuata njia bora na sahihi za uvunaji.

Ahsanteni............

Prepared by:

Marcodenis E. Misungwi. Agriculture Extensionist.

Sunday, October 9, 2016

HEALTH FIT ADVICE, EAT AND STILL BE FIT.


Research Shows: Ginger Destroys Prostate Cancer, Ovarian And Colon Cancer Better Than Chemotherapy.
Numerous people around the world have known and used the incredible health properties of ginger.

Besides being a common spice added to foods, it has also been considered to be a natural remedy for numerous various illnesses. Nowadays, the modern science has confirmed this capacity of ginger, and studies suggest that it has an immense power in the treatment of cancer.

According to the Journal of Toxicology and Food Chemistry, ginger contains two substances, known as  gingerols and paradoles, which help the prevention of cancer. Yet, scientists have shown that than conventional cancer treatments, such aschemotherapy.

Ginger destroys Colorectal Cancer.

At the conference of Cancer Prevention Research in 2003, scientists showed that ginger efficiently prevents colorectal cancer. Yet, there are numerous studies which have confirmed the same.

The Journal of Nutrition published a study in 2015 which showed that despite preventing colon cancer, ginger also destroys colon cancer cells. Therefore, this amazing root can be of great help to people who suffer from colorectal cancer, as well as those who would use it as cancer prevention.

Ginger Treats Ovarian Cancer.

Angiogenesis is the condition of onset of cancer, and it greatly determines its growth and development. Therefore, if you manage to prevent the infection of the ovaries, you may successfully prevent the cancer development.

The "BMC Complementary and Alternative Medicine" published a study which found that the ginger root has active ingredients with powerful anti-angiogenic properties, which can efficiently prevent the development of cancer.

Furthermore, the experiment of a scientist from the University of Michigan conducted at the American Association for Cancer Research showed that ginger effectively destroys cancer cells and is even a better alternative than chemotherapy, as the cancer cells in the ovaries do not develop resistance to it.

Additionally, the ginger therapy causes fewer side effects, does not cause drug resistance, and leads to less toxicity than the conventional treatments.

Ginger kills Prostate Cancer Cells.

The British Journal of Nutrition published another study which indicated that the extract of ginger successfully prevents the growth of prostate cancer cells. What's more, researchers suggest a dose of 100 mg ginger per kilo of body weight.

The findings of the study suggest that the ginger extract reduces the tumor growth by 56%.Also, ginger does not affect the development of healthy cells in the body, which is not the case with the conventional cancer treatment.

The conclusion was that it was the first report that offered a detailed explanation of the anti-carcinogenic activity "in vivo" or "in vitro" of the ginger extract in the therapeutic management of prostate cancer in humans.

Researchers also confirmed that it is more effective than chemotherapy, as it does not affect the healthy body cells. Furthermore, they have proved that ginger provides the same effects in the case of ovarian cancer as well.

Multiple studies have provided evidence that ginger efficiently prevents numerous cancer types and destroys the cancer cells in the colon, prostate, and ovaries.

Yet, the best thing about it all is that it does not cause detrimental side effects, as it destroys only the affected cells, and has no effects on the healthy ones. This means that this natural cancer treatment does not poison the body and only improves health.

Hence, you should start using ginger as a medicine as soon as possible, so make sure you incorporate it into your daily diet and use it regularly. In this way, you will prevent cancer, and even treat the existing disease, and enjoy numerous health benefits as well.

The recommended daily amount of ginger is anything up to 4 grams, while pregnant women should not take more than 1mg daily.

Finally, make sure you lead a healthy lifestyle, consume a healthy diet, and exercise regularly, in order to promote your wellbeing, and prevent cancer and other health problems.

Prepared by:

Marcodenis E. Misungwi

Agriculture Extensionist in the help of World Health and Wellness.

Sunday, October 2, 2016

MAFANIKIO YA MAIS HA SIO ELIMU TU, UTHUBUTU, KUSTAHIMILI NA UJASIRI WA MAAMUZI.


✍Ukichunguza katika jamii, utabaini kuwa sehemu kubwa ya matajiri ni wale ambao wana elimu ndogo ama hawakusoma kabisa.

👉Katika miji na maeneo yote; wenye majengo ya maana, wenye makampuni makubwa, wenye utitiri wa malori na mabasi, wenye maduka makubwa ni wale wa "darasa la saba" au wale ambao hawakuingia darasani kabisa

📚 Wasomi wengi wana maisha ya kawaida yaani yale ya kiwango cha kubadilisha mboga, wakijitahidi sana wanaishia kujenga nyumba za kuishi  na magari mawili ya kutembelea (tena kwa mikopo!).

👉Wapo wasomi wengi tu wanaoishi kimasikini, kwa lugha ya kistaarabu tunasema wana maisha ya kuungaunga. Kiukweli idadi ya wasomi walio matajiri ni ndogo sana.

👉Lakini Umasikini wa wasomi wengi umeanzia huko shuleni na vyuoni wanakopatia usomi wao. Madarasani kuna mambo mawili wanafundishwa wasomi ambayo ndio yanayowaroga

Hii inachangiwa na mambo mawili:-
👇
I. Wameelimishwa na kuaminishwa kwamba yule anaepata maswali yote kwa usahihi ndio anaonekana amefaulu. Ukikosea unahesabika kuwa u mjinga na wenyewe wanaita umefeli

👉Hata hivyo katika maisha ya kawaida hasa kwenye mchakato wa kutafuta hela, kujaribu na kukosea ni sehemu ya mafanikio

👉Kadiri unavyojaribu na kukosea mara nyingi ndivyo unavyojifunza na ndivyo nafasi ya kutajirika kwako inakuwa kubwa!

📚Wasomi wengi kwa sababu ya "mentality" ya kuogopa kukosea huwa hawapendi kujaribu biashara kwa hofu ya kushindwa kuiendesha, na huamua kufa kimasikini wakitegemea mishahara pekee kwa sababu mishahara ndio pato lao la uhakika
👇
II. Madarasani kunahimizwa ubinafsi badala ya umoja. Angalia namna mitihani inavyofanyika. Kila mwanafunzi anafanya mtihani peke yake, na ukikutwa unaangalizia ama mnasaidiana na mwenzio ndani ya chumba cha mtihani mtapata adhabu kali ikiwemo kufutiwa mtihani!

👉Katika maisha ya kawaida hasa ya kusaka fedha, unahitajika ushirikiano mkubwa sana, baina yako na wadau, wateja, wafanyakazi wenzio, marafiki n.k. Kwa kifupi unatakiwa kuwa na Networking ya kutosha.

✋Huwezi kufika mbali kiuchumi kama utakuwa na "mentality" ya ubinafsi unaosisitizwa madarasani!

Simaanishi kusoma hakuna maana, isipokuwa ninakwambia: Kama ukipata nafasi ya kusoma, soma kwa bidii; lakini usibebe kila wanachokulisha madarasani; ukakileta huku mtaani.

Mwandishi maarufu wa vitabu vya uhamasishaji motivational books katika kitabu chake maarufu cha Rich Dady, Poor Dady anauliza swali hili:

"Does School prepare children for the real life" ni swali la msingi sana tunalopaswa kujiuliza hapa. Na pia katika kitabu hicho hicho anasema:

"Get with the times! Look around the richest people didn't get rich because of their Education"

Mtaani panahitaji akili ambayo ni tofauti na hiyo iliyopimwa kupitia kukariri ya vitabuni, mwishoni wanakuzawadia makaratasi yaitwayo vyeti.

Ukitaka kufanikiwa ungana na waliofanikiwa wakuelekeze jinsi gani wamefanikiwa.

Hii habari haitaki hasira, vumilia tu na jiongeze.

Prepared by:

Marcodenis E. Misungwi

Agriculture Extensionist.

Wednesday, September 28, 2016

KILIMO BORA CHA UFUTA

UTANGULIZI

Ufuta (simsim/sesame) ni zao la kibiashara ambalo mbegu zake zina kiasi kikubwa cha mafuta kiasi cha asilimia 45 hadi 55.Na zao hili linaweza kulimwa maeneo mengi ya Afrika mashariki na Tanzania.Ni zao ambalo linatowa mafuta yenye thamani kubwa na hivyo kulifanya zao bora la biashara.

HALI YA HEWA INAYOFAA KWA KILIMO CHA UFUTA

Zao hili linawezwa kulimwa katika maeneo yanayopata mvua kidogo.Maeneo ya ukanda wa chini kutoka usawa wa bahari hufaa zaidi kwa kilimo cha ufuta.Pia nyanda za juu ambazo ni chini ya mita 1500 hufaa kwa kilimo cha ufuta.Mfano kwa Tanzania unaweza Ukalima ufuta katika mikoa ya Morogoro, Lindi, Manyara, Dodoma, Iringa na mkoa mpya wa Songwe katika maeneo ya bonde la Songwe wilaya mpya ya Songwe.

UDONGO UNAOFAA KWA KILIMO CHA UFUTA.

Ufuta ustawi vizuri katika maeneo yenye udongo mwepesi mweusi na usiotuamisha maji,udongo tifutifu ni mzuri kwa kilimo cha ufuta,Pia ufuta unawezwa kulimwa katika udongo wowote lakini usiotuamisha maji.Ufuta hufa haraka kama maji yatatuama kwa muda mrefu shambani.

AINA ZA UFUTA

Kuna aina kuu mbili za mbegu za ufuta:

1) MBEGU ZA ASILI

Wakulima wengi hupanda mbegu za asili, mbegu ambazo zilianza kulimwa miaka mingi iliyopita.Mbegu hizi nyingi zina mavuno kidogo, kati ya 300kg-500kg kwa ekari na huchukua muda mrefu kukomaa Huchukua siku 140 hadi 180.

2) MBEGU ZA KISASA

Mbegu hizi zinakomaa kwa muda mfupi na hutowa mavuno mengi, wastani wa 500kg hadi 800kg kwa ekari kama shamba litaandaliwa, litapandwa na litatunzwa vizuri. Mbegu hizi huchukua siku 105 hadi 140 kukomaa.Mfano wa mbegu hizi ni Naliendele 92,Lindi 202,Ziada 94 na Mtwara 2009.

UPANDAJI WA UFUTA

Shamba la ufuta ni budi likatuliwe na kulimwa vizuri kabla ya kupanda,hata hivyo pia unaweza kupanda bila kukatua lakini mavuno yatapungua kidogo. Inashauriwa kupanda ufuta kwa mistari kwa vipimo vifuatavyo. Sentimeta 50 kwa 10 au 50 kwa 20 kama utapanda kwa kutumia mistari ya kuchimba vijifereji vidogo katika mstari na kudondosha mbegu hizo katika vifereji hivyo (Drilling method) na kwa kuacha mche mmoja mmoja kwa kila shina.
Pia sentimeta 50 kwa 30 au 60 kwa 30 kwa kuacha miwili kwa kila shina. Kwa Mbegu ya Asili Unaweza Kupanda kwa sentimeta 70 kwa 30 kwa Kuacha Miwili kwa Kila shimo.Fukia mbegu kwa sentimenta 2.5 hadi 5.

MUDA WA KUPANDA

Muda mzuri wa kupanda ufuta ni mwanzoni mwa msimu wa kilimo yaani Mwishoni mwa mwezi November hadi katikati kwa mwezi Januari.

MATUMIZI YA MBOLEA

Ufuta ni zao ambalo halihitaji matumizi makubwa ya Mbolea.Japokuwa hustawi zaidi katika udongo wenye rutuba ya kutosha.Kama utapanda katika ardhi isiyo na rutuba ya kutosha basi unaweza kutumia mbolea kiasi kidogo Mbolea kama vile UREA na BOOSTER.

MATUNZO NA PALIZI

Miche ya ufuta ni midogo na laini sana hivyo inahitaji palizi mapema hasa katika kipindi cha majuma manne ya kwanza. Pia katika kipindi hiki unatakiwa kupunguza miche iliyosongamana. Kadri utavyochelewesha palizi na kupunguzia mimea mapema ndivyo unavyoifanya mimea isikuwe vizuri na kujipunguzia kipato chako.

MAGONJWA YA UFUTA

Magonjwa makuu ya ufuta ni madoa ya majani na kuoza matawi na shina. Zuia magonjwa haya kwa Kupanda mbegu bora na kwa kutokupanda ufuta katika ardhi inayotuamisha maji, pia itawezekana kubadilisha shamba usilime ufuta katika shamba lililolimwa msimu uliopita.

WADUDU WANAOSHAMBULIA UFUTA

Kuna wadudu wengi wanaoshambulia ufuta kama vile vibaruti (Ambao hushambulia hatua ya mwanzo kabisa ya miche iliyoota ya ufuta ambapo vibaruti hula majani ya mwanzo ya mmea mara tu yanapojitokeza). Pia Aphids hushambulia ufuta kwa kufyonza maji katika majani ya mimea hivyo kupelekea kukauka kwa majani ya mmea.
Pia wapo funza wa majani ambao hula majani ya mimea na pia hufunga majani ya ncha ya mimea na kuzuia ukuaji wa matawi wa mimea,wadudu hawa ni hatari zaidi kwani wanazuia kutengenezwa kwa vitumba vya ufuta.

Kuzuia vibaruti:

Kabla hujapanda mbegu yako changanya na dawa ya tunza au gaucho. Pia panda mbegu bora na fanya mzunguko mazao shambani. Wadudu wengine wakijitokeza tumia dawa kama karate, dimethoate, Twigathoate, duduall, duduba na dawa nyingine za wadudu kabla wadudu hawajasababisha madhara makubwa shambani.

UVUNAJI

Ufuta uliokomaa tayari kwa kuvunwa utaonesha mabadiliko ya majani yake na shina na matawi yatabadilika rangi yake na kuwa njano au kahawia au yataanza kukauka,pia vitumba vya mwanzo vitaanza kubadilika rangi yake na kuanza kukauka hivyo utatakiwa ukate ufuta mapema kabla vitumba havijakauka na kupasuka.Vuna ufuta wako kwa kukata matawi ya ufuta na kuyafunga katika matita ya saizi inayokufaa ila yasiwe matita makubwa sana ambayo hayatakauka katikati kwa urahisi yasimamishe matita yako kuelekeza juu kisha acha yakauke kwa wiki mbili hadi nne kutegemea na ukali wa jua.vitumba vikisha kauka na kupasuka tandika mkeka au turubai na yageuze matita yako katika mkeka na turubai hapo ufuta utamwagikia katika mkeka au turubai lako,kuupata ufuta unaokwama katika matita piga piga kidogo tita unapoligeuza. Kisha Peta ufuta wako na kuuweka katika Vyombo safi vya kuhifadhia.

SOKO

Soko la ufuta kwa kiwango kikubwa kinauzwa nje ya nchi, matumizi ya ndani ni machache sana. Na hasa wanunuzi wakubwa ni India na wauzaji wakubwa kwa ukanda wetu huu ni wakenya, ndo ma exporter wakubwa ingawa inawezekana hata hawazalishi kiwango kikubwa cha ufuta kutuzidi. Kipindi cha mavuno bei ya ufuta hufikia hadi 1800/= kwa kilo na ukiadimika hufikia hadi 2200/= kwa kilo na dumu la lita 20 hufikia hadi kilo 18.

Prepared by

Marcodenis E. Misungwi

Agriculture Extensionist.

Tuesday, September 27, 2016

KILIMO BORA CHA MCHICHA

Mchicha ni mboga za majani na maua yake hutumika katika kutengeneza mchuzi rojorojo. Mbegu za mchicha ni chakula safi kwa watoto wachanga. Mbegu husagwa na kutengenezwa uji na zaidi ya hayo pia mchicha huweza kumwongezea mkulima kipato.

MAHITAJI YA HALI YA HEWA KWAAJILI YA KULIMA MCHICHA.
Mchicha unahitaji maji ya kutosha katika kipindi chake chote cha ukuaji hadi kuvuna. Vilevile mchicha huhitaji udongo wenye rutuba ya kutosha na wenye kuhifadhi maji.

UTAYARISHAJI WA SHAMBA
Tengeneza shamba la mchicha kwa kutifua ardhi na kulainisha udongo wenye kina cha sentimeta thelathini. Weka mbolea ya samadi debe moja katika kila mita moja ya mraba. Panda mchicha katika matuta yenye upana wa 90cm-100cm.

AINA ZA MBEGU

· Amaranthus hybridus huu ni mchicha wenye majani mekundu na mbegu zake ni nyeusi.

· Amarantus africana ni mchicha wenye majani ya kijani na mbegu zake ni ni nyeusi.
· Amaranthus hypochondriacus ni mchicha wenye majani ya kijani na mbegu zake ni njano hasa mbegu zake hutumika kutengeneza uji wa watoto wachanga.

· Amaranthus dubius ni mchicha wa kienyeji na Aspinosus ni mchicha wenye miba mingi.

UPANDAJI
· Changanya mbegu za mchicha na mchanga kwa uwiano wa 1:3, 1:4, 1:5 au 1:6 ili kurahisisha upandaji.
· Mchicha upandwe katika tuta kwa mistari yenye nafasi ya sentimita thelathini.

· Funika mbegu kwa kutumia udongo uliolaini na tandaza nyasi kavu baada ya kupanda ili kutunza unyevunyevu na toa matandazo baada ya siku tatu hadi tano tangu siku ya kupanda.

· Pandikiza mchicha kwa nafasi ya sentimeta kumi na tano kwa ishirini.
· Mwagilia maji ya kutosha.

KUKUZIA
Tumia mbolea ya samadi iliyolowekwa kwenye maji kwa muda wa masaa ishirini na nne kumwagilia mchicha wako ili kupata mavuno mengi zaidi. Tumia kiasi cha debe moja kwa kila mita moja ya mraba.

NAMNA YA KUDHITI WADUDU WAHARIBIFU

Adui mkubwa wa mchicha ni wadudu aina ya mafuta au kitaalamu zaidi huitwa spinach aphids ambao hufyonza utomvu wa mchicha na kusababisha majani kujikunja , mchicha kusinyaa na kunyauka. Kudhibiti wadudu hawa mwagilia mchicha wako kutumia chombo kinachotoa maji mithili ya mvua kitaalamu kinaitwa "watering can" ili kuwadondosha wadudu hao.

Wadudu wengine ni kitambazi ambacho hula majani ndani kwa ndani hivyo tumia mwarobani kunyunyuzia majani ili kuwaua wadudu hao waharibifu.

MAVUNO

Mchicha huwa tayari kuvunwa baada ya majuma 3 hadi 6 tangu kupandwa au kupandikizwa. Uvunaji huweza kuendelea kwa muda wa miezi 2 hadi 3 kutegemeana na namna utakavyoamua kuuvuna mchicha wako.

KIASI CHA MAVUNO

Kila mita moja ya mraba huzalisha kiasi cha 4kg hadi 5kg za mchicha. Hii inamaanisha kuwa utapata kiasi cha tani 20 hadi 40 kwa hekta moja ya mchicha.

NAMNA YA KUHIFADHI MCHICHA KWA SIKU NYINGI ZAIDI

· Baada ya kuvuna funga mashina ya mchicha na weka katika chombo chenye maji kwa kufanya hivyo unaweza kuhifadhi mchicha kwa muda wa masaa 24 yaani siku moja.

Ili kuhifadhi mchicha kwa zaidi ya miezi 4 fanya kama ifuatavyo:-

· Vuna mchicha wako kisha usafishe vizuri
· Funga katika mafungu.
· Chemsha maji mpaka yachemke.
· Tumbukiza mafungu ya mchicha katika maji yanayochemka kwa muda wa dakika 1 hadi 2.

· Kausha vizuri chini ya kivuli na utunze mchicha wako katika sehemu isiyo na unyevunyevu.

Hapo utakuwa na uhakika wa kuuza mchicha wako supermarket na kuusafirisha hata nje ya nchi.

Prepared by:

Marcodenis E. Misungwi

Agriculture Extensionist.

Monday, September 26, 2016

JINSI YA KUTENGENEZA CHAKULA CHA VIFARANGA WADOGO

Leo nataka nikuonyeshe jinsi ya kutengeneza chakula cha vifaranga wadogo yaani wa wiki 1 hadi wiki 4.

Mahitaji muhimu katika utengenezaji wa chakula cha vifaranga kilo 100.

Pumba ya mahindi 40kg,

Mahindi ya kuparaza 10kg,

Mashudu ya alizeti 20kg,

Dagaa 24kg,

Unga wa mifupa 5 kg,

Chokaa 1/4kg,

Chumvi iliyo sagwa 1/2kg

Chikpremix 1/4kg.

Hayo ndio mahitaji muhimu katika uandaaji wa chakula cha vifaranga kilo 100.
Ndugu kumbuka kuwa unaweza kutengeneza chakula hicho kwa ajili ya vifaranga wako na pia unaweza pia ukafanya biashara ya kuuza chakula cha kuku kwa kuanza na hicho cha vifaranga wadogo, jua kuwa katika jamii sio kila mfugaji anaweza kutengeneza chakula cha kuku kuna wengine wanaweza lakini hawana mda wakutengeneza na pia kuna wengine hawajui kabisa jinsi ya kutengeneza, Ndugu msomaji wa mtandao huu ningependa utajirike na ufugaji kwa kuanzia na biashara ya uuzaji wa vyakula vya kuku. Leo anza kutengeneza hicho kwa kilo 100 unaweza kutengeneza ata kg 200kg, 300kg, 500kg ata 1000kg cha kufanya wewe ndiye unapaswa kuongeza mahitaji kwa kadri uwezavyo .

Prepared by:

Marcodenis E. Misungwi

Agriculture Extensionist.

Tuesday, March 15, 2016

KIROBA- KUURUDISHA MUHOGO KATIKA CHATI.

Habarini ndugu zangu wapenzi wasomaji wa mtandao wangu, poleni na shughuri za ujenzi wa taifa.   Hatukuwa pamoja kwa wiki kadhaa kutokana na majukumu mbali mbali.

Mhogo ni zao linalookoa jamii nyingi hapa nchini hasa inapotokea ukame. Linahimili ukame na pia hutumika kuandaa bidhaa zingine ambazo zinatokana na nafaka kama vile Unga, chips , keki na Maandazi.

Tanzania ni nchi ya nne kwa uzalishaji wa muhogo barani Afrika, ambapo inakadiriwa huzalisha takribani tani milioni 5 Kwa mwaka ikiwa ni wastani wa tani 8 kwa hekta.
Karibu hekta 670,000 za ardhi ya kilimo zinatumika kuzalisha Muhogo. Muhogo ni zao muhimu la chakula baada ya Mahindi. Linachangia Karibu 15% za chakula nchi nzima.
Inakadiriwa zaidi ya kaya 1.3 milioni zinajishughulisha na kilimo cha Muhogo nchini hasa mikoa ya Pwani na kanda ya Ziwa.

Kuanzia miaka ya katikati ya 90 zao hili lilianza kupotea kutokana na kuingia ugonjwa wa Batobato na Mnyauko. Wataalamu walihangaika kukabiliana na magonjwa haya bila mafanikio.

Njia rahisi ya kukabiliana na magonjwa haya ni kuruhusiwa kutumika kwa technologia ya GMO, Genetic Modified Organisms. Kutokana na technologia ya GMO, watafiti kutoka katika kituo cha utafiti cha Nliendele huko Mtwara chini ya Dr. Godfrey Mkamilo, wamefanikisha kupatikana kwa mbegu bora ya Muhogo aina ya KIROBA ambayo haiathiriwi na magonjwa haya hatari. Mbegu ameshafanyiwa utafiti na majaribio ya kutosha na wakulima hasa wa mikoa ya Lindi na Mtwara wameikubali na kuipenda sana maana inazaa sana, mikubwa mikubwa na siyo michungu.
Mbegu hii huzaa tani 25-30 kwa hekta na huvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.

Zao la muhogo likiimarishwa vizuri litasaidia kuimarisha usalama wa chakula hasa maeneo ya ukame nchini.

Note:
          Kuna kemikali iitwayo Cynogenic Glucoside ambayo inaweza kuwa sumu endapo mihogo haitaandaliwa vizuri. Kiwango cha sumu hii ni kikubwa kwenye mihogo michungu.

Imetayarishwa na kuandikwa na
Marcodenis E. Misungwi.
Agriculture Extensionist.