Mtandao huu ni kwa ajili ya kuelimishana juu ya Kilimo na Mifugo na changamoto zake. Karibu tujifunze wote.
Thursday, May 29, 2014
SHAMBANI SOLUTIONS: WHY AGRICULTURE NEEDS YOUNG PEOPLE
Saturday, May 24, 2014
UANDAAJI WA KAHAWA BORA.
Ubora wa kahawa ndio uti wa mgongo kwa upatikanaji wa bei nzuri. Ili mkulima apate bei nzuri, ni muhimu azingatie kanuni zote kilimo bora cha kahawa. Kwa kufanya hivyo, atakuwa amejijengea mazingira imara ya kuzalisha kahawa ya madaraja ya juu itakayompatia bei nzuri.
Mambo ambayo mkulima anatakiwa kufanya ili apate kahawa bora ni;
1. Kuheshimu na kutekeleza kanuni zote za kilimo bora cha kahawa, bila kuruka mojawapo.
2. Vivyo hivyo, ni budi kuzingatia kanuni zote za utayarishaji wa kahawa, kuanzia hatua ya kuvuna shambani, hadi inapopelekwa kwenye kituo cha mauzi.
Leo katika Makala hii nitajielekeza zaidi kueleza na kufundisha kanuni za utayarishaji bora wa kahawa kuanzia hatua ya uvunaji. Mkulima hana budi kuelewa kwamba atakuwa amejenga na kuimarisha msingi mzuri kwa ubora wa kahawa yake iwapo atakuwa makini katika kutekeleza kanuni zote za kilimo bora cha kahawa. Hali kadhalika kwa kuwa mwangalifu katika kutayarisha kahawa kabla haijauzwa, mkulima atakuwa analinda na kuhifadhi ubora ambao umeshajengeka. Kufanya vinginevyo atakuwa anavuruga mafanikio ya kazi nzuri ya awali.
Sifa nzuri ya kahawa inatambulika kirahisi kwa sura, umbo, uzito wa punje, na kadhalika kwa uonjo/ladha yake. Sifa hizi zinajengeka au kuharibika kutokana na uimara au udhaifu wa matunzo shambani. Kahawa hupangwa katika madaraja mbalimbali kulingana na vigezo hivyo vya ladha, sura, umbo na uzito wa punje.
(i) Madaraja ya kahawa ni; kutoka juu kwenda chini ( kunakoambatana na kupungua kwa thamani) AA, A, PB na C kulingana na kiwango cha sifa zilizotajwa hapo awali.
(ii) Kahawa ya madaraja ya chini AF, TT, T na F ni nyepesi licha ya kupungukiwa na sifa nyinginezo za kahawa bora katika madaraja ya juu.
Ni dhahiri kwamba, kahawa ya mkuluma aliyezingatia kanuni zote za kilimo bora, itakuwa katika madaraja ya juu na atapendelea kutunza na kuhifadhi ubora huo ili apate bei nzuri zaidi.
Lengo la kuhifadhi ubora wa kahawa litafikiwa kwa kutekeleza kwa uangalifu kanuni zote bora za utayarishaji wa kahawa.
KANUNI ZA UTAYARISHAJI BORA WA KAHAWA NGAZI YA MKULIMA.
KUCHUMA; Hakikisha unachuma matunda yaliyoiva ambayo ni mekundu sawasawa.
Usichume zile zenye rangi nusu-nyekundu nusu-njano au ya mchanganyiko wa kijani kibichi. Ikiwa hizo zimechumwa kwa bahati mbaya, zitengwe kabla ya kuanza zoezi la kumenya, la sivyo zitaharibu ladha na sura ya kahawa baadaye.
KUMENYA; Kahawa imenywe siku ile ile inapochumwa, kuhakikisha kuwa ile sukari iliyo kwenye ganda la nje haipenyezi ndani hadi kwenye punje, kwa kuwa itaharibu uonjo. Mashine ya kumenyea iwe safi na irekebishwe vizuri ili isije ikaminya punje. Tumia maji mengi na safi wakati wa kumenya. Ni vyema buni zimwagwe kwenye maji na kukorogwa ili zile nyepesi na zilizo haribika zielee. Hizo ziondolewe ziwekwe kando ili zimenywe peke yake. Maelea yote yaondolewe na kushughulikiwa peke yake. Baada ya kumenywa kahawa isafishwe kiasi na maelea yote yaondolewe.
KUVUNDIKA; Hatua hii ni ya kuondoka ute (mscilage) unaozunguka kila kila punje. Baada ya kusafisha kahawa iliyomenywa, ni muhimu ivundikwe katika matangi masafi yaliyo yaliyotengenezwa kwa saruji. Vifaa vya Aluminium/ chuma kama vile masufuria, pia vinafaa. Kamwe usitumie vifaa vya mbao. Kahawa ilundikwe pamoja na kusonganishwa na siyo kutandazwa. Kahawa hiyo ifunikwe kwa gunia safi ili isifikiwe na mwanga wa jua au mvua. Kahawa ivurugwe mara kwa mara ili yote iweze kuvunda kwa pamoja. Yafaa kufanya hivyo walau mara mbili kwa siku.
Baada ya masaa 24, kahawa hiyo ioshwe kwa maji kwa maji yanayotiririka na ifunikwe tena. Hakuna muda wa kanuni wa kuivundika kahawa. Tofauti za hali ya hewa katika maeneo tofauti huharakisha au kuchelewesha kahawa kuvunda. Uvundikaji wa kahawa huwa umekamilika pale punje ikibonyezwa kwa vidole hukwaruza, na ule ute unaonatanata unakuwa umetoweka. Vinginevyo kutokamilika kwa uvundikaji au kuvunda nusunusu kutaifanya kahawa yako kuwa na ladha/uonjo, harufu na sura ngeni ambayo vinachangia sana katika kupungua kwa ubora wa kahawa.
KUSAFISHA; Safisha kahawa kwa kutumia maji safi na panga katika madaraja. Ondoa punje nyepesi na masalia yote ya maganda. Hakikisha unasafisha kahawa yako vizuri hadi ute wote unaonatanata umeisha kwenye punje. Kahawa yako sasa iko tayari kuanikwa.
KUANIKA NA KUPANGA KATIKA MADARAJA.
(a) Kuanika
Baada ya kusafishwa, kahawa ianikwe kwenye chekecheke zilizoinuliwa kiasi cha meta moja kutoka usawa wa ardhi. Ardhi chini ya chekecheke iwekwe katika mazingira safi. Kamwe nyasi zisiachwe kuota kukaribia chekecheke.
Sambaza kahawa kwenye chekecheke katika kina cha inchi moja. Hakikisha unyevu unanyauka na kuisha kwenye ngozi ya punje (skin drying). Siku ya kwanza kuanika endelea kuvurugavuruga kwenye chekecheke na kuifunika kahawa vipindi vya jua kali sana ili isikauke kupita kiasi na pia kuizuia kupata vumbi. Ikiwezekana, baada ya ngozi ya juu kukauka, hamishia kahawa kwenye jafafa (kitambaa cha gunia- hessian cloth). Utagundua kuwa kahawa yako imekauka vizuri utakapobonyeza punje kwa vidole isibonyee, na rangi ya punje kubadilika na kuwa nusu kijani na nusu kijivu. Ukitumia chombo cha kupimia unyevu kitaonyesha unyevu usiozidi 13% kwenye punje.
(b) Kupanga katika madaraja.
Katika ngazi hii, hatua hii ni ya awali tu. Wakati kahawa ikiendelea kukauka, ondoa buni, punje zilizo na mabaki ya maganda na zilizobadilika rangi. Pia ondoa zilizo nyepesi na zile zilizo babuka zitunzwe na hatimaye kuuzwa pekee.
KUHIFADHI GHALANI
Kahawa sasa iwekwe kwenye magunia safi na kuhifadhiwa katika ghala safi na lenye nafasi ya kutosha kuruhusu mwanga na mzunguko wa hewa.
Kwenye ghala, magunia ya kahawa yapangwe juu ya mbao zilizoinuliwa ili yasigusane na ardhi. Hakikisha ghala halivuji maji na wala halina hali ya unyevu. Kamwe ghala lisiwe na bidhaa nyingine zozote kama vyakula, viungo vya chakula, madawa ya mimea au ya mifugo.
Kahawa ipelekwe kwenye kituo cha mauzo katika mazingira hayo hayo ya usafi.
MWISHO
Mkulima atakayezingatia kanuni kwa makini atakuwa amezalisha kahawa bora na kuitunza vizuri hivyo kujihakikishia bei nzuri.
Kwa kuwa uzalishaji wa kahawa duniani unaendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka, njia pekee ya kuboresha mapato yetu ni kuongeza uzalishaji na kuendelea na jitihada za kuimarisha na kulinda ubora wa kahawa yetu.
Imetayarishwa na kuandikwa na Marcodenis E. Misungwi kwa ushirikiano na Tanzania Coffee Board, TCB.
Friday, May 23, 2014
KILIMO RAHISI CHA UYOGA KWA WAKULIMA WADOGO WADOGO.
Namna ya kuotesha Uyoga.
Kabla ya kuzalisha uyoga inabidi kuwa na chumba chenye paa ambalo litazuia jua, mvua na vumbi. Chumba hiki kinatakiwa kiwe na sakafu inayohifadhi unyevunyevu pamoja na sehemu ya giza ambayo ni muhimu kwa kuotesha utando wa Uyoga. Mkulima wa kawaida anaweza kutumia kasha kama sehemu ya giza.
Hatua muhimu katika kuotesha Uyoga baada ya kupata mbegu ni kama ifuatavyo:
. Kusanya masalia ya mazao kama vile mabua, majani ya mpunga, ngano, Pumba za mpunga au mahindi, masalia ya miwa baada ya kukamua n.k
Vitu hivi hutumika kama mali ghafi kwa kuoteshea Uyoga.
. Mabua, Majani ya Mpunga au Migomba yakatwe kwa urefu usiozidi sentimeta 6, au urefu wa vidole kwa kutumia panga au kisu.
. Loweka mali ghafi kwenye maji ya kawaida kwa muda wa siku nzima ( saa 24).
. Kisha yachemshwe kwa muda wa saa 2 ili kuua vijidudu pamoja na vimelea vilivyomo.
. Ipua na umwage maji yote halafu tandaza kwenye kichanja kisafi ili yapoe bila kuchafuliwa na vumbi au vijidudu.
. Kisha jaza mali ghafi hii katika mifuko ya nailoni tayari kwa kupanda mbegu.
Namna ya kupanda.
Kuna aina mbili za upandaji;
AINA YA KWANZA
Chukua mfuko wa nailoni, weka tabaka ya mali ghafi ya kuoteshea kiasi katika mfuko halafu tawanya mbegu juu yake.
Baada ya kuweka mbegu, weka tena tabaka nyingine ya kuoteshea na kuweka mbegu juu yake.
Endelea kuongeza tabaka kwa namna hii mpaka ifikie ujazo wa robo tatu ya mfuko.
NB: Tabaka la mwisho la juu lazima liwe la vioteshea.
AINA YA PILI
Changanya mali ghafi ya kuoteshea ( baada ya kuchemsha na kupoa) na mbegu ya uyoga katika uwiano wa 1:25 ( mbegu : mali ghafi ya kuoteshea).
Kwa uyoga aina ya Mamama ( Pleurotus spp), kisha mchanganyiko huu ujazwe katika mifuko ya nailoni. Mifuko hii iwe ya ukubwa wa sm 20 kwa sm 40 ambamo unaweza kujaza kilo 1-1.5 ya mali ghafi ya kutosha.
Katika njia zote mbili, funga mifuko na toboa matundu kwenye mifuko yenye kipenyo cha sm 6 hadi 10 kwa kila mfuko.
Zingatia:
(i) Matundu yawe mengi ili kuingiza hewa ya kutosha ndani ya mifuko.
Uyoga ni Kiumbe hai, hivyo unahitaji kupumua.
(ii) Ukishanunua mbegu, kama hupandi kwa muda huo, hifadhi kwenye jokofu. Kama huna jokofu, nunua mbegu baada ya kuandaa kila kitu. Mbegu za uyoga zinaweza kuota vizuri hata zikikaa nje ya jokofu kwa siku mbili.
(iii) Waweza kutumia chupa moja yenye ujazo wa mililita 300 kwenye kilo 15 za mali ghafi ya kupteshea. Hakikisha unamaliza mbegu yote kwenye chupa kwani ikibaki itapata maambukizo ya vimelea.
(iv) Hakikisha unaponunua mbegu iwe ni nyeupe. Mbegu ambayo siyo nyeupe ni dalili za maambukizo ya vimelea. Vingine na hivyo haifai kupandwa.
Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na Marcodenis E. Misungwi, Agriculture Extension Officer at Mbozi District Council.
MATUNZO YA ZAO LA UYOGA.
Weka mifuko kwenye chumba cha giza. Kwa mkulima wa kawaida waweza kutumia kasha lisilopitisha mwanga kama chumba cha giza.
Acha mifuko humo kwa muda wa siku 14-21 bila kufunua ili ukungu mweupe uweze kutanda vizuri.
Utando wa uyoga ukishatanda vizuri kwenye mali ghafi ya kuoteshea, hamishia kwenye chumba cha mwanga na hewa ya kutosha kisichopigwa jua.
Katika chumba chenye mwanga. Mifuko inaweza kuwekwa kwenye meza, chanja ya waya au miti. Mifuko pia inaweza kuning'inizwa kwenye kamba.
NB: Unaweza kunyunyizia maji juu ya mifuko yaliyochemshwa na kupoa, mara tatu au zaidi kwa siku.
Tahadhari:
Usizidishe maji kwani maji yakiwa mengi sana yanaweza kuozesha uyoga.
Aina nyingi za uyoga huanza kutoa vichwa siku 2-3 baada ya kuwekwa kwenye mwanga.
UVUNAJI WA UYOGA.
Uyoga huwa tayari kuvunwa siku tatu baada ya vichwa kuonekana.
Uyoga uvunwe kwa mkono kwa kushika katikati ya shina la uyoga, kisha zungusha hadi uyoga ung'oke.
Usiondoe kichwa peke yake katika kuvuna uyoga kwa kubakiza shina huzuia uyoga mwingine kutokea.
Tuesday, May 13, 2014
ZIARA YA KUBADILISHANA UZOEFU KWA WAKULIMA KATIKA MRADI WA AGRA - AFYA YA UDONGO.
Katika mchakato wa kilimo kuna wadau wengi wanaohusika katika kuhakikisha kwamba mkulima ananufaika na kilimo kwa kuongeza tija kwenye uzalishaji na katika kuongeza kipato chake na kupanua pato la taifa kwa ujumla.
Mojawapo ya wadau wanaofanya kazi moja kwa moja na kwa ukaribu na mkulima ni Watafiti, ambao kazi yao kubwa ni kutafiti uwezekano wa kuongeza kipato katika uzalishaji kwa kutumia njia mbali mbali ambazo zitaleta tija mashambani.
Kuna vituo vingi vya utafiti hapa nchini ambapo walau kila kanda ina kituo cha utafiti. Ili mkulima aweze kuzalisha mazao ya kutosha, hana budi kushirikiana kwa karibu na watafiti ili kuweza kuendana na chochote kinachotolewa na watafiti katika kuendeleza kilimo chake.
Kituo cha utafiti uyole ni jituo kinachohudumia nyanda za juu kusini, katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Ruvuma na Rukwa. Katika Mradi wa AGRA, kitengo cha Afya ya Udongo ( Soil Health Project) kinachosimamiwa na Kituo cha Utafiti Uyole chini ya Mtafiti William Mmari na timu yake, wameweza kufanya kazi moja kwa moja na wakulima kwa kuwashirikisha Wagani na Wakulima wenyewe kwa pamoja.
Katika Mradi huu mbinu mbali mbali za uzalishaji zinatumika na wakulima wenyewe ndio wanaohusika na kushiriki moja kwa moja shambani.
Katika kubadilishana uzoefu kwenye maeneo yanayosimamiwa na mradi, watafiti wamefanya ziara kubwa ya kutembeleana ambapo lengo kuu ni kujaribu kuonyesha uhalisia wa matumizi ya Mbolea ya Minjingu Mazao.
Mbolea ya Minjingu Mazao imekuwa na changamoto nyingi sana tangu kuingia kwake sokoni. Imeweza kutekwa na wanasiasa na kuiondolea uhalisia wake. Mbolea hii haikufanya vizuri ilipoingia sokoni, na yawezekana kwa sababu ya elimu duni waliyokuwa nayo wakulima katika matumizi ya Mbolea hiyo. Baada ya kuonekana hivyo watengenezaji wa Mbolea hiyo waliamua kuiongezea virutubusho zaidi na kuibadilisha jina na sasa inaitwa Minjingu Mazao.
Serikali imeamua kuwatumia Watafiti na Wagani kwa kutumia mashamba darasa. Katika mashamba darasa ya Mradi kwa kweli yamefanya vizuri kwa kutumia Minjingu Mazao kama yanavyoonekana kwenye picha hapo juu. Wakulima waliohudhuria walishuhudia na kuamini.
Mbolea hii si mbaya kama inavyochukuliwa na baadhi ya wanasiasa na wakulima. Lakini kitaalamu ni Mbolea nzuri na ina faida za ziada kwenye udongo. Inaweza kuonekana haina ubora endapo mkulima hatafuata kiwango halisi cha uwekaji kwenye shamba.
Matumizi ya mbolea yoyote yanasimama kwenye kiwango cha kutumia shambani. Minjingu inatakiwa 120kg kwa ekari moja au kwa hesabu ya rahisi kwa mkulima ni mifuko 2 kwa ekari. Kosa lililofanyika mwanzo mwanzo ni uelewa wa wakulima wa jinsi ya kutumia Mbolea hii. Walikuwa wakitumia kwa mazoea ya DAP ambayo hutumika 50kg ama mfuko mmoja kwa ekari na matokeo ni kushindwa kukidhi hitaji kwa mmea.
Pia katika kutembeleana kwenye ziara hii ambapo nami nilikuwa mmoja wapo, tulitembelea katika mashamba ya vijiji viwili katika kata ya Isansa wilaya ya Mbozi ambavyo ni Isansa na Mpito. Na katika kijiji cha Mpito tuliweza kutembelea shamba la Mkulima mmoja ambaye alihudhuria kama shuhuda wa Minjingu Mazao ambapo amelima shamba lake la takribani eka 2 na robo tatu hivi kwa kutumia mbolea ya Minjingu Mazao na akakuzia mkuzio wa kwanza kwa kutumia Minjingu mazao hiyo hiyo na mkuzio wa pili akatupia kidogo UREA mifuko 2 tu. Matokeo katika shamba hili ni mazuri na yanaridhisha sana.
Wito wangu kwa wakulima ni kwamba mnashauriwa kufuata ushauri wa wataalam katika kutumia Pembejeo.
Imetayarishwa na kuandikwa na Marcodenis E. Misungwi, Afisa Kilimo na Mifugo.
Friday, May 2, 2014
KILIMO HIFADHI CHA MATANDAZO NA KUPANDA BILA KULIMA.
Uchumi wa soko huria umesababisha ongezeko kubwa la gharama za mbolea za viwandani, zana, madawa ya kuulia wadudu pamoja mbegu bora. Katika hali hii ni wazi wakulima ( hasa wadogo wadogo ) hawataweza kumudu ushindani iwapo wataendelea kutumia pembejeo za viwandani.
Uharibifu wa mazingira ( mmomonyoko wa ardhi, mgandamano wa udongo au udomgongo mfu ) unachangiwa na ongezeko la watu pamoja na gharama kubwa ya zana na pembejeo. Tunalazimika kubadilisha mtazamo wetu juu ya mazingira na mfumo sahihi/endelevu wa Kilimo. Zipo njia za asili za kurutubisha udongo na vilevile Kilimo cha jadi cha kutunza mazingira.
Wakulima wanashauriwa kupunguza utegemezi wa mbolea za viwandani kwa kujitengenezea mbolea yao wenyewe mashambani kwa kupanda na kufunika ardhi kwa mimea ya mikunde.
MATANDAZO.
Matandazo ni mimea hai au mabaki inayopandwa kwa madhumuni ya kufunika udongo mwaka mzima.
Kanuni ya kufunika udongo kwa mimea jamii ya mikunde, nyasi na mingineyo ndiyo muhimu zaidi na ya msingi kuliko zote.
Mizizi ya matandazo ina uwezo wa kutindua na kulainisha udongo kwa kiwango kikubwa zaidi ya majembe tunayokatulia. Kilimo cha matandazo kinaondoa ulazima wa kukatua.
KUPANDA BILA KULIMA.
Inawezekana kupanda kwenye matandazo bila kuyalima kwa kutumia zana maalum. Hizi ni pamoja na Mwuo ( Dibbler ), Jembe la mkono, Kipanzi mkono ( Jab Planter), Kipanzi komoleo matandazo ( Direct seeder ).
KANUNI ZA KILIMO HIFADHI MATANDAZO.
- Funika udongo wakati wote kwa mimea hai au mabaki yake.
- Usichome moto, usihamishe mabaki ya mazao, usichungie mifugo holela.
- Usilime/uaikatue udongo.
- Panda kwa kukomelea kwa zana maalum.
- Kilimo cha mzunguko.
Mikunde > Nyasi > Mikunde Miti > Nyasi.
HATUA ZA KILIMO HIFADHI.
1. Andaa shamba.
* Punguza uchachu wa udongo kama upo kwa Mbolea ya Minjingu, Chokaa au mmea uitwao Lupins.
* Tindua au katua kina kirefu kuondoa Mgandamano wa udongo kama upo.
* Panda Matandazo yasiyooza haraka na yenye mazap au mabaki mengi. Matandazo yanaqeza kupandwa kwa mfumo wa Kilala bora, Mchanganyiko au Kupokezana.
2. Fyeka na laza matandazo kwa Nyengo, Gogo au Kisu Kidekuzi ( Chopping knife roller ) juma 1-2 kabla ya kupanda zao kuu.
3. Pulizia dawa ya kuua wadudu ( kama ni lazima ).
4. Panda kwenye Matandazo kwa Kipanzi maalum. Weka mbolea ya asili ya kupandia.
5. Palilia magugu nachache yatakayoota kwa kung'olea au kupiga dawa ya magugu.
6. Rutubisha kwa kuongeza kiwango cha mbolea za viwandani ( kwa mwaka wa kwanza ). Dhibiti magonjwa/wadudu hasa kwa dawa za asili.
7. Kwa msimu unaofuata, rudia mzunguko kwa kilimo cha mzunguko wa mazao.
MANUFAA YA KILIMO HIFADHI.
i. Kuongeza mboji na rutuba ya udongo. Hatimaye mahitaji ya mbolea za viwandani hupungua.
ii. Kupunguza mahitaji ya nguvu kazi na muda kwa hadi 60%. Hii inatokana na kutohitajika kukatua na haro.
iii. Kuongeza kiwango cha mvua kupenya kwenye ardhi na udongo kutunza unyevunyevu. Athari za vipindi vya ukame au mvua kupita kiasi ni ndogo zaidi katika kilimo cha matandazo.
iv. Kupunguza mmomomonyoko wa udongo. Matone ya mvua hukingwa yasidondoke kwenye udongo n kuusambaratisha. Uchafuzi wa maji katika mito hupungua.
v. Kupunguza gharama za uzalishaji mazao na kuongeza faida. Baadhi ya Matandazo ( Mucuna, Marejea, Desmodium, Vetch ) yana uwezo wa kudhibiti magugu sugu kama ndago.
vi. Kupunguza uchakavu wa zana, mitambo na mafuta kwenye kilimo.
vii. Kutindua na kulainisha ardhi iliyo gandamana. Mizizi ya baadhi ya mimea ya matandazo ( Mbaazi, Fiwi, Nyonyo, Utupa, Marejea pori ) inaweza kwenda chini hadi futi nne.
CHANGAMOTO ZA KILIMO HIFADHI.
. Ni shida kuwashawishi wakulima, wataalam wa ugani, na hata watafiti kubadili mtazamo na kukubali Kilimo Hifadhi.
. Inahitaji kiwango cha juu cha nidhamu na usimamizi wa kilimo.
. Kuzuia uchungaji holela wa mifugo.
. Kuzuia utayarishaji wa mashamba kwa kuchoma moto.
. Matandazo ni makazi salama ya Panya na Nyoka.
Kwa hiyo ndugu zangu wakulima na wadau mbalimbali wa kilimo, ni vema kuweza kubadili mawazo na mtazamo wa kifikra katika kuongeza kipato kwa gharama nafuu.
Imetayarishwa na kuandikwa na Marcodenis E. Misungwi, Agriculture Field Officer.
Monday, April 28, 2014
MICHAKATO YA KUHIFADHI VYAKULA MBALIMBALI KWA KUKAUSHA.
Ukaushaji wa vyakula mbalimbali hutumiwa na wakulima wengi kama njia mojawapo ya kuepusha uharibifu wa mazao na kuviwezesha kutumika kwa muda mrefu. Yafuatayo ni maelezo ya michakato mbalimbali inayotumika kuvikausha vyakula hivyo.
MBOGA: Majani ya kunde, Matembele, Mchicha na Majani ya Maboga.
* Chambua mboga vizuri na chuma majani machanga.
* Safisha mboga vizuri
* Chemsha kwenye maji ya moto kwa dakika 1-5 (inategemeana na ugumu wa mboga, laini ni dakika chache na ngumu ni dakika nyingi) kwenye maji yenye chumvi ili rangi ya kijani iaitoke.
* Chuja kwa kutumia chekeche
* Anika nje kwenye chombo safi kama mkeka, ungo, chekeche. Epuka kukausha kwenye jua kali, anika kivulini na jua la asubuhi kabla halijawa kali.
* Kausha mpaka mjani yavunjike kwa urahisi na geuza geuza mara kwa mara.
* Weka katika chombo kinacho funika kama debe, kopo n.k.
MATUNDA: Nyanya, Ndizi, Maembe, Tende, Zabibu, Ukwaju, Nanasi.
* Tumia kisu kisichopata kutu kwa kukata matunda ili kuzuia matunda kuwa meusi.
* Osha na katakata vipande vyembamba. Ndizi ni lazima umenye.
* Tende, zabibu, ukwaju unaanika hivyo hivyo nzimanzima.
* Ndizi chemsha kwa dakika 5 katika maji ya chumvi ili kuzuia rangi mbaya isitokee.
* Kausha taratibu kwenye jua la kiasi mpaka zikauke.
* Weka katika vyombo visivyoingiza unyevu.
Kabeji
* Osha na katakata vipande vyembamba
* Chemsha kwa dakika 2 tu kwenye maji yenye chumvi.
* Chuja na anika kwebye chombo safi mpaka zikauke.
* Weka katika vyombo visivyoingiza unyevu.
Kisamvu
* Angalia majani laini na twanga.
* Chemsha katika maji yenye chumvi kidogo kwa dakika kumi ili kupunguza sumu hasa kama umechuma majani ya muhogo.
* Kausha katika chanja kwa kutumia mkeka safi, ungo au chekeche.
* Weka katika chombo kisichoingiza unyevu.
MIZIZI: Viazi vitamu na mihogo.
* Tumia viazi au mihogo iliyokomaa.
* Menya, katakata vipande vyembamba kidogo.
* Safiasha au chemsha katika maji kwa dakika tano.
* Kausha katika chanja na katika hali ya usafi.
* Ikikauka weka kwenye chombo safi kisichoingiza unyevu.
Imetayarishwa na Marcodenis E. Misungwi, mtaalam wa kilimo na mifugo.
Sunday, April 27, 2014
SABABU ZINAZOWEZA KUATHIRI CHANJO KUTOA KINGA KWA KUKU INGAWA WAMECHANJWA.
Zipo sababu ambazo kama mfugaji hakuzingatia kanuni na taratibu za uchanjaji kuku ugonjwa unaweza kutokea.
. Ratiba ya chanjo.
Kutokufuata ratiba ya utoaji chanjo (Vaccination Programme) iliyopendekezwa na mtaalam wa mifugo wa eneo au kanda husika, kunaweza kusababisha kuku wasipate uwezo wa kujikinga na ugonjwa huo ingawa watakuwa wamechanjwa. Hivyo inashauriwa kufuata ratiba ya utoaji wa chanjo iliyopendekezwa kitaalam.
. Utunzaji mbaya wa Chanjo.
Chanjo iliyohifadhiwa katika joto kali hupoteza uwezo wa kufanya kazi. Vile vile kuweka Chanjo kwenye freezer huathiri uwezo wa Chanjo husika.
Inashauriwa Chanjo kuhifadhiwa kwenye hali ya ubaridi wa joto kati ya nyuzi joto 2°C-8°C hasa kwenye friji.
Kumbuka kwamba kuna baadhi ya chanjo kwa sasa zimepigwa marufuku kusambazwa kwa kuonekana kuchakachuliwa na kupoteza ubora wake wa kutibu. Chanjo iliyozuiwa ni ya "Matone" inayozuia ugonjwa wa Kideri. Ni vema ndugu mfugaji uwe mfuatiliaji wa mambo kila wakati.
. Ugonjwa
Iwapo kuku tayari wameshapata virusi vya ugonjwa husika, wanaweza wakaugua ugonjwa huo hata kama watachanjwa chanjo ya ugonjwa huo.
Kwa hiyo basi kabla hujawachanja kuku wako wachunguze kwanza kama hawana dalili ya kuugua, lakini la muhimu kuliko yote ni kuzingatia ratiba ya uchanjaji maana yawezekana wakawa hawaonyeshi dalili ya kuugua lakini kumbe wadudu wakawa wameshaingia.
. Kutofuata masharti ya watengenezaji wa Chanjo kuhusu matumizi ya Chanjo.
Mbali na maelekezo ya matumizi ya chanjo ambayo hutolewa na wataalamu wa mifugo au wauza madawa ya mifugo wanaotambulika katika kutoa huduma hiyo. Ni muhimu pia kuzingatia masharti ya mtengenezaji chanjo husika.
. Usafirishaji na utoaji Chanjo.
Usafirishaji wa chanjo katika mazingira yasiyofaa huathiri nguvu ya Chanjo, pia utoaji wa Chanjo yenyewe na wataalam wa mifugo au madawa ya mifugo huathiri zoezi lote (Vaccination Procedure) la uchanjaji wa kuku. Inaahauriwa Chanjo isafirishwe kwenye chombo au kifaa chenye ubaridi au chenye uwezo wa kuhifadhi joto linalotakiwa, pia kuzingatia taratibu zote za mwenendo wa kuchanja kuku.
. Lishe duni.
Chakula ambacho kina viinilishe duni vinavyohitajika kukidhi afya bora ya kuku husababisha kuku kuwa dhaifu, hivyo huwa mwili wa kuku hauna uwezo wa kujikinga na magonjwa. Hivyo ni vema kulisha chakula cha kuku chenye ubora unaokidhi mahitaji ya afya ya kuku.
. Utumiaji wa dawa za tiba na chanjo kwa pamoja.
Hii pia huathiri uwezo wa Chanjo kufanya kazi kwenye mwili wa kuku. Ni vema kutowapa chanjo na dawa za tiba (antibiotics) kwa wakati mmoja. Inashauriwa kutowatibu kuku siku mbili kabla na baada ya chanjo kutolewa pia wapewe vitamini kama Vitalyte, Poultry antistress, Vitastress, Stressvita n.k.
. Vijisumu (mycotoxins).
Hivi ni vijisumu ambavyo huwa kwenye chakula cha kuku kilichohifadhiwa vibaya kama vile unyevunyevu au kwenye tandiko chafu, hivyo kuku akila chakula chenye vijisumu hivi hupunguza kinga za mwili kupambana na magonjwa, kwani vijisumu hivi hushambulia sehemu muhimu ndabi ya mwili wa kuku ambazo hujihusisha na kinga na magonjwa. Hivyo inashauriwa vyakula vya kuku vihifadhiwe kwenye sehemu isiyokuwa na unyevunyevu au joto kali, pia nafaka zinazotumika kutengeneza chakula cha kuku changanya na vitu vinavyosaudia kupambana na vijisumu hivi. Waweza kutumia Farmacid premix na mycobind kwenye chakula.
. Usumbufu (Stress)
Kuku waliopata usunbufu siku chache kabla au baada ya chanjo huwa wanapungukiwa na uwezo wa kupokea chanjo ili kujikinga na ugonjwa, usumbufu unaweza kuwa msongamano (overstocking), kukata midomo (beak trimming), kuwahamisha kuku kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Hivyo epuka usumbufu kwa kuku unapokaribia muda wa kuwapa Chanjo ili kufanya chanjo ifanye kazi vizuri.
Imetayarishwa na Marcodenis E. Misungwi, Mtaalam wa Kilimo na Mifugo.
Friday, April 18, 2014
UTUNZAJI BORA WA MAZAO BAADA YA KUVUNA.
Katika mchakato wa uvunaji, ni kipindi cha kuwa makini sana maana unaweza ukazalisha vizuri lakini ukaja kupoteza kiasi kikubwa wakati wa mavuno.
Katika kuhakikisha kwamba mazao yanakuwa katika ubora na hali nzuri kwa mlaji (consumer), wadau katika mchakato huu lazima waunganishe nguvu za pamoja. Hebu tuwatambue wadau hawa na wajibu na majukumu yao katika mchakato huu.
(i) Mkulima
(ii) Serikali
(iii) Maafisa Ugani
(iv) Wauza Pembejeo (Stockissts)
Wajibu wa Mkulima
- Kulima kwa kufuata kanuni bora za kilimo.
- Kuvuna na kuandaa mazao
- Kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu.
- Kuwasilisha matatizo yao kwa wagani ili waweze kujadiliana jinsi ya kuyatatua.
- Kutumia mbinu za kienyeji zenye kuleta mafanikio.
Wajibu wa Serikali
- Kutunga na kusimamia sheria na sera (mfano sheria ya Dumuzi)
- Kuwawezesha wagani kuwasaidia wakulima (mafunzo)
- Kufanya utafiti
- Kutoa ruzuku au mikopo midogo midogo kwa ajili ya kuendeleza hifadhi ya mazao.
- Kutunga na kusimamia Sera ya Masoko.
Wajibu wa Wagani
- Kuwatembelea Wakulima na kujadiliana kuhusu changamoto mbalimbali na jinsi ya kuzitatua.
- Kuwaunganisha wakulima na watoa huduma mbalimbali.
- Kuunganisha wakulima na watafiti.
Wajibu wa wauza Pembejeo
- Kuwauzia wakulima Pembejeo bora ikiwa ni pamoja na viuatilifu vilivyosajiliwa na vyenye ubora unaostahili
- Kutoa elimu kwa wakulima.
MAANA HALISI YA UHIFADHI NA UPOTEVU WA MAZAO.
* Uhifadhi ni kitendo cha kuweka mazao yako sehemu maalum kwa muda maalumu kabla ya kuuzwa au kutumika.
* Upotevu wa mazao ni hali ya kupungua thamani kwa mazao kutokana na sababu mbalimbali kama vile kusinyaa, kunyauka, kuliwa na wadudu, kuibiwa au kupotea.
Madhumuni ya kuhifadhi
. Kwa ajili ya chakula
. Kwa ajili ya biashara
. Kwa ajili ya biashara
. Kwa ajili ya mbegu
AINA YA UPOTEVU WA MAZAO.
Upotevu wa mazao unaweza kutokea kwa namna mbalimbali kama:
1. KUPUNGUA UZITO
Kuna aina nyingi za visababishi na vingi ni vile vinavyokula mazao hasa wadudu na wanyama kama Panya. Aidha uvunaji usio na umakini huacha mazao mengi shambani na hivyo uhifadhi kuanza na kiasi pungufu kuliko ilivyokusudiwa.
2. KUPUNGUA KWA UBORA
Visababishi vikuu ni wadudu wanaokula, wanaochafua, au shughuli inayovunja au kuharibu punje, kuchafua mazao kwa aina yoyote au kuoza, kusinyaa, kutoa harufu n.k
3. UPOTEVU WA VIINI LISHE
Visababishi vikuu ni vile vinavyokula viini vya punje ambavyo ndivyo vyenye virutubisho na vitamini. Kadhalika hifadhi duni.
4. UPOTEVU WA MAPATO
Hutokana na yote yaliyotajwa hapo juu ambapo matokeo yake ni zao kupata ndogo kwenye soko na hivyo uchumi wa mkulima kuwa duni.
5. UPOTEVU WA NGUVU YA UOTO KWENYE MBEGU.
Visababishi ni hifadhi duni na vyote vilivyotajwa hapo juu.
Katika mzunguko mzima wa uvunaji, kuna ngazi mbalimbali za upotevu ambazo ni;
- Kuvuna
- Kusafirisha
- Kukausha
- Kupukuchua/kupura
- Kupepeta/kuchambua
- Kupanga madaraja
- Kuweka dawa ya kuua wadudu
- Kuhifadhi kwenye vifaa au maghala
- Kutumia kwa chakula au kuuza
- Kusinsika.
Hebu basi tujadili sasa njia za kuweza kudhibiti upotevu wa mazao baada ya kuvuna.
DHANA SHIRIKISHI YA UDHIBITI WA VISUMBUFU.
Aina za wadudu waharibifu:
i. Dumuzi
ii. Fukusi wa mahindi
iii. Mende mwekundu wa unga
iv. Wadudu jamii ya nondo/vipepeo
v. Visumbufu wengine ni wanyama waharibifu wakiwemo Panya.
UDHIBITI WA VISUMBUFU AINA YA WADUDU.
. Udhibiti kwa njia ya asili (Cultural control)
. Udhibiti kwa kutumia viuatilifu (Chemical control)
. Udhibiti kwa kutumia nguvu ya binadamu (Physical control)
. Udhibiti husishi (Intergrated Storage Management)
Katika udhibiti kwa njia ya viuatilifu, inatakiwa mkulima awe mwangalifu kuangalia viuatilifu sahihi na viwango vya kutumia. Kadhalika matumizi salama ya viuatilifu na tahadhari yatasisitishwa.
Mambo mengine muhimu ambayo yanapaswa kuzingatiwa katika matumizi ya viuatilifu ni pamoja na;
. Kukauka kwa nafaka
. Usafi wa nafaka
. Kuchambua nafaka
. Kugawa zao
. Viwango sahihi
. Kutumia viuatilifu ambavyo havijakwisha muda wake
. Usafi na hali ya ghala au vyombo vya kuhifadhia
. Ukaguzi wa mara mara wa nafaka na ghala.
Sasa tuangalie jinsi ya ktumia viuatilifu aina ya vumbivumbi. Kabla ya kuanza shughuri nzima ya kutumia kiuatilifu (dawa), mambo muhimu ya kuzingatia ni;
(i) Kuhakikisha ni kiuatilifu kilichopendekezwa na wataalamu
(ii) Kusoma lebo na kufuata maelekezo kwa usahihi
(iii) Jinsi ya kupima na kujua kiwabgo kilachoshauriwa
(iv) Jinsi ya kuhakikisha kwamba nafaka imekauka kwa kiwango kinachostahili
(v) Kuzingatia mwelekeo wa upepo wakati wa kutumia
(vi) Jinsi ya kusafisha magunia au vyombo vingine kabla ya kuvijaza nafaka
(vii) Mambo ya kuzingatia katika kuondokana na vifungashio vilivyokwisha kiuatilifu pamoja na viuatilifu vinavyobaki.
(viii) Tahadhari za kiafya wakati wa kutumia viuatilifu.
Jinsi ya kutumia viuatilifu aina ya majimaji kutayarisha ghala.
Zoezi hili litazingatia mambo yafuatayo ;
(i) Tofautisha matumizi ya viuatilifu vya majimaji na vile vya vumbivumbi katika hifadhi.
(ii) Jinsi ya kuchanganya kiuatilifu cha majimaji kupata kiwango kinachostahili.
(iii) Matumizi sahihi ya mabomba ya kunyunyizia viuatilifu.
Njia mbadala kwa madawa ni kutumia vifaa visivyoingiza hewa kama vile mapipa.
Udhibiti wa Panya
Panya ni visumbufu katika kundi la wanyama, hushambulia zaidi mazao ya nafaka kuanzia shambani hadi ghalani na hupunguza kipato cha mkulima kwa kiwango kikubwa asipo dhibitiwa. Ili kuweza kumdhibiti Panya ni lazima;
- Ujue tabia za Panya
- Ujue jinsi ya kutambua maeneo wanakopita.
- Ujue sumu za Panya (sumu za kizazi cha kwanza na za kizazi cha pili).
Ujue namna sahihi ya utegaji wa Panya.
Note: aina hizo za dawa yaani kizazi cha kwanza na kizazi cha pili, kizazi cha kwanza ni dawa ambayo inaua Panya peke yake na kizazi cha pili ni ile dawa ambayo inaua mtambuka pale ambapo kuku akimdonoa Panya aliye kufa, na huyo Kuku atakufa kutokana na hiyo dawa. Zipo hadi kizazi cha tatu ingawa ni mara chache ambapo binadamu au mbwa akimula huyo Kuku, atakufa.
Kwa hiyo ndugu zangu wakulima na wote mnaotembelea kwenye blog hii, tujitahidi kadri tuwezavyo kukabiliana n upotevu huu.
Sunday, April 13, 2014
ZIARA YA KAMATI YA UCHUMI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBOZI YATEMBELEA MRADI WA BWAWA LA NANSAMA.
Jopo la waheshimiwa madiwani, Kamati ya Uchumi wametembelea mradi wa maji kwa ajili ya huduma za umwagiliaji katika kijiji cha Nansama kata ya Isansa.
Mradi huu ulianzishwa kwa uwezeshwaji kama kikundi cha kahawa Igabda na benki ya NMB chini ya kitengo chao cha Development Foundation ukigharimu Tsh. 30,000,000/= hata hivyo baada ya ujenzi kumalizika na watu kuanza kutumia, lilibomoka na halmashauri kupitia Idara ya Kilimo iligharamia ukarabati huo. Na tokea hapo mradi sasa uko chini ya halmashauri.
Kamati iliongozana na jopo la watumishi kutoka katika Idara mbalimbali hasa zinazoshabihiana na Kilimo wakiongozana na Mkaguzi wa ndani.
Kamati ilimuomba mwenyekiti wa bwawa atoe maelezo ni historia fupi juu ya jinsi mradi ulivyoanzishwa na unufaika wa wananchi katika mradi huo. Mwenyekiti alieleza kwa kifupi na kukumbushia ushauri uliokwishatolewa na mkuu wa mkoa pindi alipotembelea mradi h mwezi January wa halmashauri kuweza kuangalia uwezekano wa kulipanua zaidi ambapo sambambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa alishauri miti ipandwe kulizunguka bwawa ambalo hilo l miti limekwisha tekelezwa na miti imepandwa na inaendelea vizuri. Maswali mawili matatu pamoja na ushauri yakaulizwa.
Bi. Lydia Shonyela, ambaye alimwakilisha Afisa Kilimo na Umwagiliaji (DAICO) pia alitoa baadhi ya maelezo ya jinsi halmashauri ilivyosaidia katika mradi huo.
Baada ya hapo waliondoka kuelekea kata Ruanda.
Friday, March 28, 2014
UZALISHAJI WA MBEGU BORA ZA MAHARAGE - DARAJA LA KUAZIMIWA UBORA (Quality Declared Seed), QDS.
Mbegu ya kuazimiwa ubora (quality declared seed) huzalishwa na wakulima wadogo wadogo na vikundi vya wakulima wadogo vijijini, chini ya usimamizi wa washauri wa Kilimo wa Wilaya.
SIFA ZA MBEGU BORA/VIPIMO VYA UBORA WA MBEGU.
. Mbegu za aina moja (uhalisia wa kizazi) - Ili kuwa na sifa hii ukaguzi lazima uanzie kwenye shamba la kuzalisha mbegu.
. Mbegu safi - Zisizochanganyika na aina zingine au mazao mengine, mbegu za magugu, zisizoliwa na wadudu na uchafu kama udongo na takataka zingine.
. Mbegu zilizokomaa na kukauka vizuri - Kama zimekauka vizuri haziwezi kuoza na kuvunda, na huota vizuri pia haziwezi kushambuliwa na wadudu kwa urahisi. Hii huiwezesha mbegu ibaki na ubora wake kwa muda mrefu.
. Mbegu zilizovunwa kutoka mimea yenye afya kutoka shamba lenye mazao mazuri - Mbegu zilizovunwa kutoka kwenye mimea dhaifu haziwezi kuota vizuri na kwa wakati mmoja na mimea yake huwa dhaifu.
. Mbegu yenye afya nzuri - Mbegu ambayo haiwezi kuwa chanzo cha magonjwa. Fungu la mbegu isiyo salama kiafya isitumike kama mbegu. Vime vya magonjwa huweza kusambazwa kwa njia ya mbegu kama mbegu hii itatumika.
. Mbegu zenye uwezo wa kuota kwa zaidi ya asilimia tisini (90%).
. Mbegu za aina bora zinazokibalika (chagua aina ya mbegu kulingana na mahitaji).
. Mbegu mpya (pre-basic/foundation), isirudiwe kupandwa zaidi ya misimu miwili.
SEHEMU YA KUPANDA.
. Panda sehemu zenye udongo usiotuamisha maji na wenye rutuba.
. Panda mbegu katika maeneo yenye mwinuko wa mita 400m-1800m kutoka usawa wa bahari kwa nyanda za juu kusini.
WAKATI WA KUPANDA.
. Usipande kipindi cha mvua nyingi zinazoanza mwezi Novemba au Disemba hadi April au mei, panda mwezi Februari hadi March.
. Sehemu kavu zenye mvua ya muda mfupi kama, panda mwezi Disemba hadi Februari.
. Sehemu zenye maji ya umwagiliaji panda wakati wa kiangazi.
UPANDAJI.
. Panda kwa nafasi zinazoshauriwa sentimita 50 mstari hadi mstari na sentimita 10 mbegu hadi mbegu (50cm × 10cm).
. Tenga aina mbalimbali za mbegu kwa nafasi ya mita zisizopungua mita 3.
. Usipande mbegu katika mchanganyiko wa mazao mengine.
MBOLEA
. Weka mbolea wakati wa kupanda kama inavyopendekezwa. Mfano, mifuko 1 (kilo 50) TSP na 3/4 (kilo 40) mfuko CAN au DAP mfuko 1 (kilo 50).
PALIZI
Wahi palizi ya kwanza ndani ya wiki 2 baada ya maharage kuota na rudia tena kabla ya kuchanua. Unaweza kutumia madawa ya kuua magugu kama SATECA au Stomp.
WADUDU
. Funza wa maharage ni wadudu wanaoshambulia mimea michanga ya maharage. Funza wa maharage hawa huweza kusababisha uharibifu hadi kufikia asilimia 100 kufuatana na hali ya hewa-unyevu kidogo, rutuba kidogo, kuwepo kwa maotea ya aina ya maharage na magonjwa kwenye udongo, kurudia kupanda zao la maharage kila msimu na aina ya naharage.
Njia nzuri ya kudhibiti funza wa maharage haws ni:-
1. Kupanda mapema
2. Kupakaza mbegu dawa kama endosufan, Acephate, Murtano (mchanganyiko wa dawa ya fungas na wadudu) nasaidia kuzuia funza wa maharage na visababishi vya kuozesha mizizi.
TAHADHALI: Dawa ya Murtano ni sumu kali hivyo mbegu zenye dawa hii zisitumike kwa chakula.
3. Kunyunyizia dawa mfano Karate 5EC au Actellic 50EC ndani ya siku 4 hadi 5 baada ya maharage kuota.
4. Kupanda mbegu zenye afya kwenye udongo wenye rutuba.
5. Kupanda mbegu zenye ukinzani wa funza wa maharage.
6. Kuweka matandazo kama pumba ya mpunga husaidia kuotesha mizizi mipya n kurudisha afya ya mmea wa maharage.
MAGONJWA
Magonjwa maarufu ni ndui ya maharage, madoa pembe, kutu, magonjwa yanayosababishwa na bacteria na virusi. Mbegu iliyoambukizwa, udongo na takataka za maharage ni vyanzo vikubwa vya uambukizaji kwa magonjwa yote isipokuwa ugonjwa wa kutu ya majani.
1. Punguza athari kwa kupanda mbegu safi, zenye afya zisizo na vidonda/ magonjwa, aina zinazovumilia na kutunza shamba.
2. Panda kwa mzunguko wa mazao ya jamii nyingine.
3. Ondoa na kuchoma yaliyougua.
4. Tumia dawa zilizopendekezwa kama Kocide, Funguran, Bayleton n.k kwa kuzuia magonjwa yanayosababishwa na ukungu na bacteria.
KUVUNA NA KUTAYARISHA MBEGU.
Vuna maharage mar yatakapokauka. Kausha kwa kuanika juani, piga, peta na kausha tena juani. Unaweza kuvuna kilo 600 hadi 800 kwa ekari kabla ya kuchambua endapo utafuata kanuni za kilimo bora.
Chambua mbegu vizuri kwa kuondoa uchafu, udongo, mbegu za aina nyingine, punje zilizopasuka na zilizohafifu. Pia ondoa punje zenye vidonda/mabaka na zilizotobolewa na wadudu. Hakikisha mbegu zimekauka vizuri kabla ya kuhifadhi.
KUHIFADHI MBEGU.
Safisha vyombo au ghala na ondoa wadudu. Zuia wadudu kwa kutumia dawa za asili au za viwandani. Tumia dawa za kuhifadhia mbegu kama Actellic (gramu 100 za Actellic super Dust kwa kilo za mbegu za maharage), Murtano (gramu 300 za Murtano kwa kilo 100 za mbegu za maharage) na dawa zinginezo kwa kiwango kinachoshauriwa na wataalamu. Weka mbegu mbali na maharage ya chakula pamoja na vyakula vingine. Epuka sehemu zenye unyevu na paa zinazovuja na zuia panya. Usihifadhi mbegu kwa zaidi ya misimu miwili maana baada ya hapo uwezo wa kuota hupungua.
KUPIMA UWEZO WA KUOTA
Pima uwezo wa uotaji kabla ya kupanda. Uotaji mzuri ni wa zaidi ya asilimia tisini (90%).
Panda mbegu 100 katika kila sehemu tatu zinazofanana na zenye unyevu. Baada ya siku kumi chunguza miche iliyoota vizuri na kuihesabu.
Tumia kanuni ifuatayo:-
Asilimia ya uotaji = miche iliyoota vizuri × 100 gawanya kwa 300.
Ahsanteni sana!
Imetayarishwa na kuandikwa na Marcodenis E. Misungwi, Agriculture Field Extension Officer III, Mbozi District Council, Mbeya.
Friday, March 21, 2014
KILIMO CHA UYOGA.
UTANGULIZI.
Uyoga ni aina ya nyuzi kuvu (fungus) yenye kutofautiana na mimea mingine kwa kukosa chembe chembe zinazowezesha mimea kujitengenezea chakula yenyewe kwa kutumia hewa na mwanga.
Uyoga unaota wenyewe kwenye mashamba hasa wakati wa mvua kwenye maeneo yenye mboji nyingi. Sasa hivi nchini tunao utaalamu wa kuotesha uyoga au ndani ya nyumba au nje kwenye kivuli maalumu.
HISTORIA FUPI YA UYOGA.
Uyoga umefahamika na wanadamu tangu enzi za zamani sana. Miaka elfu nne kabla ya kuzaliwa Kristo watu walijua uyoga. Historia inatueleza kwamba watu wameanza kulima kwa utaalamu mwaka 300 baada ya kuzaliwa Kristo.
Wadadisi wa mambo wanauelezea Uyoga kufanana sana na chakula waisraeli walichokuwa wakila kule jangwani katika safari yao ya kutoka utumwani Misri.
Wakati Uyoga ukilimwa katika dunia yote, hapa Afrika na hasa kwetu Tanzania mambo yalikuwa ni tofauti kabisa. Hakuna mtu aliyesumbuka na kilimo hicho. Ni hapo majuzi tu mwaka 1993 ndipo ukulima ulianza Dar es salaam. Mwaka 1994 ukulima ulianza Arusha, mwaka 1995 ukulima ulianza huko Mbeya, na mwaka 2003 ukulima ulianza huko Kilimanjaro.
AINA YA UYOGA.
Inakadiriwa kuwa kuna aina milioni moja na laki tano (1,500,000) za nyuzi kuvu (fungus) duniani; katika hizi ni aina 64,000 ambazo zimekwisha kufanyiwa utafiti na kupatiwa maelezo ya kisayansi. Katika hizi aina 64,000, kuna ambazo zimethibitika kuwa na Uyoga halali 12,000. Na kati ya hizi ni aina 2,000 na ndizo zinazolimwa.
Katika aina 2,000 za uyoga zilizokwisha thtbitika, hapa Tanzania ni aina 40 tu.
Uyoga Mamama (Oyster mushroom).
Aina hii ya Uyoga hustawi katika nchi za Tropics. Utaalamu unaohitajika siyo mgumu. Baadhi ya aina zinazooteshwa ni hizi zifuatazo;
. Pleurotus oystreotus
. Pleaurotus sajo-caju
. Pleaurotus sapidus
. Pleurotus flabel atus - (pink oyster)
. Leaurotus Pulmonerius
. H. K. n.k
. Monkey Head
. Auriclaria
Nyingine zinazooteshwa hapa nchini kwa kiasi kidogo ni;
. Agaricus bitoquis (uyoga vifungu)
Uyoga taka ambazo ni;
. Coprinus cinereus
. Caprinus Comatus
. Lentinus edodes
. Volvoriella Volvocea
Nyingine ni;
. Ganodema lucidum
FAIDA ZA UYOGA
Uyoga una maajabu makubwa katika maisha ya mwanadamu, Uyoga ni lishe bora kwa mwanadamu, ni dawa na tiba kwa mwanadamu, ni zao la kuingizia watu kipato, ni rafiki wa mazingira pia.
LISHE
. Uyoga ni zao lenye viini lishe (amino acids) zote 22 zinazohitajika na mwili wa mwanadamu.
. Protini iliyoko kwenye Uyoga inafikia kiwango cha asilimia arobaini. Hii inalingana na protini iliyoko kwenye maziwa.
. Kuna wingi mkubwa sana wa vitamini B,C na D.
. Uyoga hauna mafuta mengi. Una asilimia tatu tu. Hivyo hauna Colestrol.
. Uyoga unayo madini yote muhimu kwa mwanadamu; phosphorus, Iron, Calcium na Potash.
TIBA
Utafiti uliofanyika siku za karibuni umethibitisha kuwepo kwa dawa nyingi ndani ya uyoga zenye uwezo wa kutibu kwa ufanisi, magonjwa ya wanadamu na mifugo. Kwa wanadamu magonjwa yafuatayo yanatibiwa;
. Kifua kikuu TB
. HIV/AID upungufu wa kinga mwilini
. Kisukari
. Shinikizo la damu
. Magonjwa ya moyo na uti wa mgongo
. Saratani
. Matatizo ya figo
. Vifo vya watoto wachanga
AJIRA
Kwa sasa hivi ajira imepungua sana katika nchi yetu. Vijana, wazee na rika lote hatuna kazi, mazao yaliyokuwa yakituingizia kipato yamepungua au yamekwisha. Nguvu kazi nyingi tuliyonayo inatumika kuuza mwanasesere na plastic zinazotoka katika nchi za nje.
Watu wengi mno tunaishi katika lindi la ufukara. Hatuna mahitaji ya msingi kama vile chakula, malazi na mavazi bora. Kufuatana na ripoti ya umoja wa mataifa, iliyoandaliwa na Professors S. T. Chang na Mshigeni wa chuo kikuu cha Namibia, mauzo ya Kahawa kwenye soko la ulimwengu kwa mwaka 1997 ni dola za kimarekani bilioni 15. Mauzo ya Uyoga yalikuwa dola bilioni 14. Katika biashara hiyo Afrika ilichangia kwa asilimia 0.3 tu.
Wataalamu hawa wanaainisha sababu nyingi zinazosababisha upungufu huu. Kubwa wanalosema ni kuwa waafrika hawajui umihimu wa uyoga katika maisha ya mwanadamu. Bei ya uyoga huko Marekani, Mashariki ya kati na Mashariki ya Mbali ni kati ya dola za Marekani tisa ($9) hadi kumi na tatu ($13). Uyoga ni zao lililo kayika mpango nafuu wa biashara ya Marekani na Afrika. Halitozwi ushuru kuingia katika masoko ya Marekani.
KUSAFISHA MAZINGIRA
Kufuatana na ripoti ya wataalamu wa chuo kikuu Kivais na Magingo ya miaka ya tisini, Tanzania inayo masalio ya kilimo na misitu zaidi ya tani milioni kumi na saba (17,000,000). Masalio haya yameachwa yakioza, au kuchomwa moto au kulishwa mchwa pamoja na mapanya. Ikiwa masalio haya yatatumika kuoteshea Uyoga, Mazingira yataboreka na uchumi utakua. Uzalishaji wa Uyoga unaanzia pale mkulima au mtumiaji wa bidhaa za kilimo na misitu anapomalizia.
MASALIO YA TAKATAKA BAADA YA KUOTESHA UYOGA.
Masalio ya takataka (vimeng'enywe) hutumika kama ifuatavyo;
. KULISHA MIFUGO
Uyoga una uwezo wa kuvunja vunja chembe chembe za vimeng'enywe na kuviboresha kuwa protini na madini mengi, kisha kufyonza hicho na kutengeneza matunda ya uyoga. Baada ya kuvuna uyoga chembechembe hizi bado zina ubora mkubwa wa chakula kwa ajili ya mifugo kama vile ng'ombe, mbuzi, nguruwe, sungura n.k. Tunao wafugaji wanaotumia vimeng'enywe hivi kulishia mifugo nao wameendelea kupata maziwa mengi.
. MBOLEA
Vimeng'enywe hivi hutumika kama mbolea shambani na katika bustani. Matokeo ya kutumia vimeng'enywe hivi yameonyesha ufanisi mkubwa.
.METHANE GAS
Tukijenga mfumo wa kutengeneza gesi kama kawaida, tunaweza kutumia vimeng'enywe hivi kutengeneza methane gas. Hii gesi itatumika kupikia, kuwasha taa na mambo mengine kama hayo. Mabaki katika zoezi hili huwa na mbolea nzuri ifaayo sana. Mazao ya shamba na bustani yaliyokuzwa kwa mbolea hii yana bei nzuri zaidi sokoni, maana yanahesabika yamezalishwa kiasili (organic agriculture).
. ZERI ( Zero Emmission Research Initiative).
Umoja wa Mataiga umeiteua Tanzania pamoja na nchi nyingine katika bara la Afrika kuendeleza na kutekeleza mfumo wa ZERI. Huu ni mfumo wa kutochafua mazingira kwa njia ya kutoa moshi. Masalia ya kilimo ba misitu yasichomwe moto bali yageuzwe kutoka hali yake na kuwa kitu kingine labda kilicho bora na chenye thamani zaidi. Masalia ya sokoni hatutayaacha yaoze bure, tutayasindika ili yaweze kuzalishia uyoga. Pumba za mpunga na kahawa hatutazichoma moto. Tutazitumia kwa kuzitengenezea chipboards, vivyo hivyo na maranda ya mbao, takataka za katani, kahawa na n.k. zitageuzwa kuwa kitu bora zaidi.
UTAYARISHAJI WA SHAMBA LA UYOGA.
Mambo ya muhimu ya kuzingatia:
. Ukubwa wa shamba
. Uwezekano wa upanuzi
. Usafi wa eneo
. Upatikanaji wa takataka za kulimia yaani vimeng'enywe
. Upatikanaji wa maji safi
. Umbali kutoka kwenye soko
Ndani ya ndani
. Hewa safi ya inayozunguka
. Joto linalotakiwa
. Unyevunyevu kwenye hewa unaotakiwa
. Carbondioxide na mwanga vinatakiwa
Shamba
Shamba la uyoga linapaswa liwe na viambatanisho vifuatavyo;
. Sehemu ya kutayarisha vimeng'enywe
. Kichanja cha kuhifadhi majani au aina yoyote nyingine ya vimeng'enywe.
. Sehemu ya kuchemshia vimeng'enywe
. Sehemu ya kupandia mbegu kwenye vimeng'enywe vilivyokwisha kuchemshwa.
. Banda kamili la kukuzia lenye sifa zilizokwisha ainishwa hapo juu
. Sehemu ya kuhifadhia uyoga uliovunwa au chumba cha baridi kutegemea na hali halisi.
UJENZI WA SHAMBA
Mkulima anashauriwa kutumia vifaa vinavyopatikana katika eneo lenyewe. Kwa mfano mkulima mwenye shamba la migomba, baai atumie marawa katika kuta na paa. Unaweza ukatumia nyasi za kawaida au majani ya mpunga, ngano na mengine ya namna hiyo, unaweza kutumia matofali mabichi, unaweza kutumia mabanzi. Ndani ya nyumba weka weupe. Hii ni chokaa au kitambaa cheupe. Hii ni kwa sababu uyoga hukua kuelekea rangi ya mazingira yaliyouzunguka. Lakini rangi nyeupe huchochea ukuaji na hudumisha usafi. Nyumba ya uyoga iwe na madirisha makubwa mazuri.
MAANDALIZI YA VIMENG'ENYWE
Kama ilivyosemwa hapo mwanzo, kila jani lililokomaa na kukauka, lafaa kuoteshea uyoga. Michanganyiko ifuatayo yafaa sana kuoteshea uyoga.
. Majani ya mpunga au migomba yenye unyevu 62%
. Pumba za mahindi unyevu 62%
. Sukari
. Chokaa
Vimeng'enywe viko vingi, mkulima anashauriwa awaone wataalamu kwa ushauri.
MAHITAJI MENGINE
Ifuatayo ni orodha ya mahitaji mengine;
. Jiko la kuchemshia
. Pipa tupu la lita mia mbili
. Mifuko ya plastic size 10" × 15" yenye uwezo wa kuhimili joto
. Viroba (polysacks) pvs ya kuweka ndani ya pipa
. Vibangili vya kipenyo cha 1.5
. Kamba au uzi wa kushonea viatu ili kufunga mifuko wakati wa kuchemsha.
. Vipande vya magazeti
. Rubber band size ya mpira wa ndana ya tairi ya baiskeli.
HATUA ZA KUFUATA KATIKA KUOTESHA
. Katakata majani yaliyokomaa na makavu katika urefu usiozidi nchi nne
. Changanya majani haya na virutubisho hapo juu i.e. pumba za mahindi, sukari na chokaa.
. Changanya sawasawa kwa kutumia maji safi ndoo tatu hadi tano.
. Zilundike mahali safi ukitengeneza mlinduko wenye kimo cha mita moja hadi mita moja na nusu.
. Funika kwa polythene paper na vitambaa vya sulphate
. Majani ya migomba yalowekwe kwa siku mbili hadi tatu kabla ya kuvundikwa
. Ziache kwa muda wa masaa 24
. Weka vimeng'enywe hivi katika mifuko ya polythene
. Weka maji lita 40 katika pipa lenye kichanja cha mbao chenye kuzuia mifuko isigusane na maji
. Bandika kwenye jiko hadi mvuke unapotoka , hesabu msaa manne.
. Ipua mifuko yako na iweke mahali safi
. Sasa ni wakati wa kufanya kila kitu kwa hali usafi. Tunatumia maji yenye detol kusuzia mikono yetu
. Otesha uyoga kama mtaalamu atakavyokuonyesha
. Baada ya siku 21 ondoa vipande vya gazeti ulivyotumia kufunika mifuko
. Baada ya siku 10 nyingine utaanza kuvuna uyoga. Uta una kwa muda wa miezi 2 hadi 3
. Weka uyoga uliovuna ili kuhifadhi ubora wa uyoga.
MAPATO YA MKULIMA
Tunaorodhesha hapa hali halisi ya mkulima wetu mwenye banda la mita tatu (3) kwa mita tano (5).
Gharama:
Majani ya mpunga Pickup moja = 25,000/-
Mifuko ya plastic 500@50 = 25,000/-
Mbegu za uyoga chupa 100@1500 = 150,000/-
Jumla = 200,000/-
Mavuno aliyopata kilo 300@3000 = 900,000/-
Toa gharama = 200,000/-
Salio = 700,000/-
Kazi hii ilimchukua mkulima huyu miezi mitatu. Ijulikane kuwa baada ya kuotesha mkulima anakagua banda kw muda mfupi sana, asubuhi saa sita na jioni. Mkulima huyu na familia yake anajipatia wastani wa shilingi 230,000/- kila mwezi kwa kulima banda moja.
MAPISHI
Mkulima na umma wote wanapashwa kujua mapishi ya uyoga.
Tunaweza kutumia uyoga kama ifuatavyo;
. Kutengeneza supu
. Kutengeneza supu ya viungo (mushroom curry)
. Kutengeneza mboga ya kawaida tunayoweza kula na vyakula vingine kama vile ugali ndizi, wali, viazi n.k.
. Tunaweza kuzindika a kutengeneza mushroom pickle (hii tutauza kwenye supermarket na mahoteli ya kawaida hasa ya kitalii)
. Tunaweza kutengeneza mushroom pizza.
MAGONJWA YA UYOGA
Uyoga ni viumbe hai. Hivyo hupatwa na magonjwa kama hali ya mazingira na utendaji haitakidhi. Kuna magonjwa ya aina kama ifutavyo;
. Bacteria
Uyoga unakuwa na rangi ya kutu. Hata mifuniko inakuwa na rangi hiyo. Ugonjwa huu unatambulika kiurahisi., kwani unakuwa unateleza.
. Fungus
Aina zifuatazo ndizo hasa zishajulikana;
. Blue mould
. Black mould
. Brown mould
. Virus
Uyoga uliopendeza unasinyaa mara moja. Unaanza kutoka jasho.
MASOKO
Mpaka sasa hoteli za kitalii zinapika uyoga wa kutoka nje uliowekwa kwenye makopo.
Ikumbukwe kuwa kwenye makopo kuna uyoga halisi kidogo sana. Pia katika supermarket za hapa nchini kuna uyoga fresh kutoka Kenya. Pia tujue kuwa majirani wetu waliotuzunguka Kenya, Uganda, Zambia na Malawi wamepiga hatua kubwa katika kilimo cha uyoga. Swali tunalopaswa tujiulize sote ni hili " Kulikoni Tanzania kuhusu Uyoga".
Tumeziona faida za uyoga. Ni bora kuliko nyama nyekundu na nyama nyeupe. Kwenye maduka ya nyama zinauzwa kilo nyingi za nyama kila siku. Badala yake tuuze uyoga kila siku.
SOKO LA NJE
Kama ilivyoelekezwa hapo juu kuna masoko ya nje. Lakini yanataka kiasi kikubwa cha uyoga. Tani kadhaa kila wiki na kila mwezi. Ili kuweza kukidhi haja hii, wakulima waunde vikundi na vyama vya ushirika ili kushughurikia jambo hili.
HITIMISHO
Andiko hili dogo lina lengo la kumuandaa Mtanzania wa kawaida aweze kuwa mkulima wa uyoga. Kamwe lisichukuliwe kama mamlaka tosha kuhusu uyoga. Sababu ni kwamba nimechagua kuzungumzia yale mepesi tu yanayoweza kumfaa mkulima wa ngazi ya mwanzo. Sayansi ya uyoga ni pana, ndefu na yenye kina.
Ahsanteni sana.
Imeandaliwa na kuandikwa na Marcodenis E. Misungwi,
Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo III, Mbozi District Council
Kwa msaada wa International Fund for Agricultural Development, IFAD.
Monday, March 10, 2014
MAGONJWA SUGU KWA KILIMO CHA KAHAWA NA UDHIBITI WAKE
Leo nitaongelea magonjwa sugu ya kahawa na udhibiti wake.
1. CHULEBUNI (CBD).
Chulebuni ama kama ujulikanavyo kama Coffee Berry Disease (CBD), ni ugonjwa mbaya sana na huenea kwa kasi. Mbuni ulioshambuliwa haufi ila mkulima anaweza kupoteza mpaka asilimia 90 ya mavuno kama hatazingatia namna bora ya kuuzuia. CBD huathiri matunda ya kahawa hasa kanda za juu na kati. Ushambuliaji ni mkubwa zaidi wakati wa masika kwani CBD hupenda hali ya unyevu na hali ya baridi.
Dalili na madhara ya CBD:
* CBD hushambulia mibuni katika hatua tatu muhimu ambazo ni:
. Maua yanapochanua.
. Punje zikiwa changa na laini.
. Punje zinazoiva.
* Madhara makubwa hutokea walati punje zikiwa changa na laini amnapo:
. Maua yaliyoshambuliwa hunyauka na kuanguka.
. Vidonda vyeusi na vilivyobonyea huonekana kwenye matunda yaliyoshambuliwa. Mengi huoza na kudondoka. Yaliyobakia hukaukia kwenye mti na kuwa chanzo cha uambukizaji kwenye mavuno ya msimu unaofuata.
* Matunda yaliyoiva hukaukia kwenye matawi na huvunwa kama buni.
* Hupunguza zao kwa asilimia kati ya 30 na asilimia 60 wakati mwingine hufikia hadi asilimia 90.
* Kudhibiti CBD hufikia hadi asilimia 35 ya gharama za uzalishaji.
* Hupunguza ubora wa kahawa kwa kiasi kikubwa.
Jinsi ya kuzuia chulebuni (CBD):
- Panda aina mpya ya kahawa inayohimili mahambulizi ya Chulebuni ambayo ni mkombozi dhidi ya ugonjwa huu hatari.
- Punguza kivuli shambani.
-Kata matawi kwa wakati na sahihi. Ondoa maotea mara kwa mara.
- Ondoa masalia ya buni zilizoathirika na teketeza kwa moto.
- Kwangua magamba kwenye mashina machafu ya kahawa.
- Anza kunyunyizia vizuia kuvu kukinga matunda machanga ndani ya wiki tatu kabla ya mvua za msimu kuanza.
- Hamasisha majirani kuzuia chulebuni kwa wakati mmoja.
2. KUTU YA MAJANI (LEAF RUST).
Kutu ya majani ni ugonjwa unaoathiri majani ya kahawa hasa kanda za chini na kati. Ugonjwa huu unaathiri kahawa aina zote; Robusta na Arabika. Kutu ya mjani isipodhibitiwa inaweza kupunguza mavuno kwa asilimia 60.
Dalili za ugonjwa:
Majani yaliyoshambuliwa hutokeza madoa madoa ya manjano chini ya jani
Madhara yake:
. Kutu ya majani hupunguza eneo la jani la kutengeneza chakula. Pia hudababisha kupukutika kwa majani yanayolisha matunda na kukuza mmea.
. Kwa hali hiyo husababisha madhara ya mmea kutoa punje ndogo zenye ubora hafifu.
. Ugonjwa ukishamiri hukausha matawi, shina zima na hatimaye mti mzima kufa.
Hali zinazochangia kuenea kwa kutu ya majani:
- Unyevu wa hewani unapokuwa zaidi ya aslimia 80 na unapoambatana na kivuli cha kupita kiasi kwenye shamba.
- Msongamano wa machipukizi na matawi katika mti wa kahawa.
Jinsi ya kudhibiti ugonjwa wa kutu ya majani:
- Punguza kivuli kuzunguka mti wa kahawa.
- Pogolea machipukizi na matawi katika mti wa kahawa.
Kuzuia kutu ya majani:
i) Panda aina mpya zinazovumilia magonjwa ya kutu ya majani na chulebuni.
ii) Boresha huduma muhimu ikiwa ni pamoja na lishe ili kuongeza uvumilivu wa magonjwa hususani ugonjwa wa kutu ya majani.
iii) Tumia viua kuvu kwa wakati na vipimo sahihi. Unyunyiziaji wa kwanza ufanywe ndani ya wiki tatu kabla ya mvua kunyesha, na kuendelea hadi mara tatu mpaka nne kwa msimu.
iv) Shirikisha na majirani kudhibiti kutu ya majani.
MAGONJWA MENGINE YA KAHAWA.
Yapo magonjwa mengine kadhaa ya kahawa ambayo umuhimu wake umemezwa na magonjwa mawili niliyozungumzia hapo juu. Ningependa kuyataja tu baadhi yake pamoja na mbinu za kuyazuia au kuyatibu.
3. BAKAJANI (Brown eye spot).
Ugonjwa huu huenezwa na kimelea aitwaye "Cercospora cofficola". Hudhibitiwa kwa utunzaji bora wa shamba na kutumia morututu.
4. UGONJWA WA PUNJE ( Bean disease).
Huu huambukizwa na kuvu aitwaye "Nematospora coryli" akienezwa na kimatira. Ili kuepukana na ugonjwa huu, ni lazima kuchukua hatua za kumdhibiti kimatira.
5. UGONJWA WA MASHINA (Scarly bark disease).
Ugonjwa huu hujulikana kama "Ukungu" kwa wakulima walio wengi, upo wa aina mbili ambao wakulima huwa wanashindwa kutofautisha na huuita kwa ujumla wake Ukungu. Aina hii ya kwanza ya ukungu huambukizwa na kuvu aitwaye "Fusarium lateritium". Hakuna udhibiti wa kitaalam mpaka sasa ila kung'oa mti mzima na kupanda upya. Ukishang'oa choma mti hapohapo na acha kwa muda angalau hata misimu miwili au mitatu kisha panda upya.
6. UGONJWA WA KUOZA MIZIZI (Root rot disease).
Huu ugonjwa unafanana kabisa na ugonjwa wa mashina, ni ukungu wa aina ya pili kama unavyojulikana na wakulima wengi. Huambukizwa na kuvu aitwaye "Armillaria mellea". Hakuna udhibiti ila kung'oa na kupanda upya baada ya muda wa misimu miwili au mitatu hivi.
Ndugu zangu wakulima, wataalam na wadau wote wa kilimo, hakikisheni mnajitahidi kwa kadri inavyowezekana kudhibiti magonjwa hayo. Kwa kufanya hivyo kutanuongezea mkulima kipato chake na pato la taifa kwa ujumla.
Ahsanteni sana!
Imetayarishwa na kuandikwa na Marcodenis E. Misungwi, Agriculture Field Extension Officer.
Sunday, March 9, 2014
WADUDU WAHARIBIFU WA KAHAWA NA JINSI YA KUWADHIBITI
1. KIMATIRA
Kimatira ni mdudu anayeshambulia kahawa aina ya Arabika. Madhara ya mdudu huyu ni kupunguza wingi wa na ubora wa kahawa. Wastani wa vimatira wawili au watatu kwa mti kwa eneo wanaweza kusababisha uharibifu wa zao kwa asilimia 45. Hufyonza matunda machanga na kusababisha kuoza. Hufyonza majani na machipukizi na kusababisha utoaji wa matawi madogo madogo na pingili fupi fupi. Dalili hizi zikionekana mkulima achunguze kuwepo kwa Kimatira kabla ya kuchukua hatua za kudhibiti. Hufyonza vikonyo vya maua na kusababisha kubadilika rangi kuwa nyeusi.
MADHARA YAKE.
. Husababisha kukauka kwa maua na kupukutika kwa matunda.
. Mashambulizi haya pia huingiza ugonjwa wa ukungu ambao huozesha kahawa na kuwa mapepe, hivyo hupunguza ubora na wingi wa mavuno.
NAMNA YA KUMDHIBITI KIMATIRA.
. Pogolea matawi mara kwa mara kadri inavyoshauriwa.
. Punguza kivuli cha miti na nigomba.
. Tumia Fenitrothion 50% EC millilita (cc) 25 za dawa kwa lita 15 za maji, Selecron 720% EC millilita (cc) 25 za dawa kwa lita 15 za maji.
. Hakikisha shamba lako linakuwa safi kila wakati ili kuzuia kuzaliana kwa mdudu huyu.
. Dhibiti wadudu hawa mara tu wanapoonekana wastani wa kimatira wawili au watatu kwa mti shambani mwako.
. Ni muhimu mashamba ya majirani yakadhibitiwa kwa wakati mmoja na shamba lako.
FAIDA ZA KUMDHIBITI KIMATIRA.
Mkulima akimdhibiti kimatira atapata faida zifuatazo;
. Atakuwa amepunguza kuzaliana kwa wadudu.
. Atakuwa ameongeza mavuno na ubora wa kahawa.
. Atakuwa amejiongezea kipato chake na kuwa maisha mazuri zaidi.
. Atakuwa ameongeza pato la taifa kwa ujumla.
2. BUNGUA MWEUPE (MAPEMBE).
Bungua mweupe au " Mapembe" ana mabawa yenye magamba meusi na kijivu. Pia ana kipapasi kirefu (antena). Wiki 1 hadi 2 baada ya mvua za vuli kuanza, mdudu huyu hutoka ndani ya shina la kahawa na kujilisha kwenye magamba machanga au matunda ya kahawa. Uharibifu wake wakati huu ni mdogo. Mdudu huyu hutaga mayai chini ya magamba kwenye shina la kahawa sentimita 30 kutoka usawa wa ardhi. Mayai huanguliwa baada ya wiki tatu na kuwa kiwavi ambaye huanza kujilisha kwa kuparua magamba ya kahawa kabla ya kutoboa na kuingia ndani ya mti ambapo hukaa kwa miaka miwili. Bila ya kumdhibiti mdudu huyu anaweza kusababisha hasara kwa kufyonza virutubisho na kufanya mti wa kahawa kuwa wa njano na baadaye kufa.
HATUA HATARI ZA MAPEMBE.
Hatua ya kiwavi cha mdudu huyu ndicho kinachosababisha madhara makubwa kwenye mti wa kahawa.
Dalili zake:
. Miti iliyoshambuliwa inakuwa na matundu kwenye mashina na hasa katika sehemu ya chini ambapo unga unga wa njano huonekana.
. Majani ya mti ulioshambuliwana kuathirika sana, hugeuka rangi ya njano na hatimae hunyauka na kufa.
Namna ya kumdhibiti:
. Njia muhimu ya kumdhibiti Mapembe ni kuutunza mti wa kahawa kuwa na afya nzuri kwa kupanda kwa nafasi iliyopendekezwa, kuweka mbolea ya kutosha, kuweka shamba katika hali ya usafi na kudhibiti wadudu na magonjwa.
. Baada ya kuvuna, kwangua magamba ya shina la kahawa (usawa wa goti toka ardhini) kwa kutumia gunzi la mahindi, ili kupunguza mazalia ya mdudu huyu, pia hufanya mayai na viwavi vyake kuonekana kwa urahisi na kushambuliwa na wadudu maadui wa mdudu huyu.
. Ua kiwavi wa bungua mweupe kwa kumchokonoa kwa waya ndani ya shimo.
. Vutia sisimizi watakao mla bungua kwa kuweka mafuta ya wanyama kwenye tundu.
. Kata miti iliyoshambuliwa sana (stumping), na kama lava amepekecha kuelekea chini, mtoe kwa waya.
. Paka chokaa, udongo au majivu ili kukausha mayai yasianguliwe kwenye shina na matawi.
. Nyunyiza mkojo wa ng'ombe uliovundikwa kwa siku 14 ili kuua au kufukuza wadudu hao.
. Kagua shamba na kamata na kuwaangamiza hasa mvua za vuli zinapoanza.
Mambo muhimu ya kuzingatia:
Ni muhimu mashamba ya jirani yakadhibitiwa kwa wakati mmoja ili kuzuia mapembe kuhamia mashamba hayo.
3. RUHUKA.
Ruhuka ni mdudu hatari ambaye huishi kwenye mibuni na mimea jamii ya mikunde, ambayo huwa ni mbadala wakati matunda ya kahawa hayapo. Mdudu huyu hushambulia zaidi mibuni aina ya Robusta na Arabica kwenye ukanda wa chini. Madhara ya mdudu huyu huendelea mpaka ghalani. Asipodhibitiwa anaweza kusababisha uharibifu wa zao shambani mpaka asilimia 90.
Dalili muhimu, uharibifu na madhara yake:
. Matunda mabichi au yaliyoiva huwa na tundu moja au zaidi kwenye kitovu cha tunda.
. Punje zilizoshambuliwa hubadilika rangi na kuwa kijani cha bluu. Katika hali hii viwavi huwepo ndani ya punje.
. Matundu yaliyotobolewa huweza kuwa njia ya kupenyeza ukungu na bacteria na kupunguza ubora wa zao.
. Ruhuka huendelea kushambulia punje ghalani na hivyo kushusha ubora wa kahawa.
Namna ya kumdhibiti Ruhuka:
. Epuka kuotesha miti ambayo inaficha hawa wadudu wakati usio msimu kama Lantana camara.
. Punguza kivuli cha shambani.
. Pogoa matawi inavyoshaushauriwa.
. Chuma kahawa mara kwa mara (kila baada ya siku 14) ili kahawa isikauke juu ya mti na hivyo kuzuia masalia ya matunda yenye Ruhuka.
. Okota matinda yote yaliyoanguka shambani wakati wote, na ondoa matunda yote yaliyobaki kwenye kahawa baada ya msimu. Chimba shimo na ufukie matunda hayo. Kwa kufanya hivyo unakatisha mzunguko wa maisha ya ndudu huyu.
. Weka matandazo ili kuendeleza wadudu marafiki wanaokula Ruhuka, hii pia husaidia kuozesha matunda yaliyodondoka chini.
. Chunguza kuwepo kwa Ruhuka katika miezi ya Februri na Machi. Akiwepo nyunyizia dawa za asili kama mwarobaini na utupa. Uchunguzi ukionyesha kuendelea kuwepo kwa Ruhuka, nyunyizia sumu za viwandani kama vile Thiodan 35EC au Dursban 48EC (15mls kwenye lita 20 za maji). Hii ifanyike kabla ya Ruhuka kuingia ndani ya punje.
. Tumia njia za kiasili kumdhibiti Ruhuka kwa mfano mtego wa chupa kwa kutumia kileo kama vile gongo, mbege, rubisi na konyagi.
. Hakikisha kwamba dawa inapigwa miezi 4 kabla ya kuvuna kahawa. Ni vyema mashamba ya majirani pia yadhibitiwe kwa wakati mmoja na shamba lako.
Faida za kumdhibiti Ruhuka:
. Kuongeza wingi wa kahawa.
. Kupunguza hasara na kuongeza kipato.
. Kupunguza uwezekano wa kupata sumu ya ukungu (OTA).
4. KIDOMOZI.
Kidomozi ni nondo mdogo mweupe ambaye mchana hujificha chini ya majani ya kahawa na kuruka usiku. Kidomozi hushambulia zaidi majani ha kahawa aina ya Arabika. Mashambulizi yanayofanywa na wadudu hawa hupunguza mazao kwa asilimia 8-10. Nondo wa kidomozi hutaga mayai juu ya majani ya kahawa na huangua viwavi wadogo ambao huharibu mjani kwa kuacha makovu ya kahawia.
Dalili zake:
. Majani yaliyoshambuliwa yanakuwa na mabaka ya rangi ya kahawia na juu ya jani linaonekana lina mabaka ya ukavu.
. Endapo ukifumua kovu kwa kutumia waya mwembamba utaona viwavi wembamba na weupe.
Madhara yake:
. Mashambulizi ya viwavi hawa hupunguza eneo la majani linalotengeneza chakula cha mmea na kusababisha majani kupukutika.
. Kupukutisha majani husababisha mti wa kahawa kushindwa kutengeneza chakula cha kutosha kujilisha na hasa kulisha matunda.
Namna ya kumdhibiti kidomozi:
. Zingatia usafi wa shamba (kukata matawi, kukatua shamba na kuweka matandazo).
. Punguza kivuli shambani ili mwanga wa jua upenye kwa asilimia 60.
. Tumia dawa ya asili kama mkojo wa ng'ombe kwa uwiano wa 1:4 (mkojo:maji) kwa kunyunyizia kwenye shamba la kahawa.
. Tumia Selecron 720EC cc 25 za dawa kwenye lita 15 za maji, Dursban 48%EC tumia cc 30 za dawa kwa lita 15 za maji. Decis (Deltamethrin) 2.5%EC tumia cc 6.5 kwa lita 15 za maji, Furadan 5G (Carbofuran) tumia gram 30 kwa mti kila mwanzoni mwa mvua (Dawa hii ya carbofuran iwekwe chini kwenye mizizi).
. Dawa hizi zitumike wakati nondo 30 au zaidi wanapoonekana kwenye mti.
. Tumia dawa hizi baada ya wiki moja nondo wa mdudu huyu wanapokuwa wengi. Rudia tena kupiga dawa baada ya wiki 2 hadi 3.
. Badilisha dawa za kudhibiti mara kwa mara kwani utumiaji wa aina moja ya dawa husababisha wadudu hawa kuwa sugu.
Faida za kumdhibiti kidomozi:
Mkulima akidhibiti kidomozi atapata faida zifuatazo:
. Atakuwa amepunguza kuzaliana kwa wadudu hawa
. Atakuwa ameongeza wingi wa mavuno na ubora wa kahawa.
. Atakuwa amejongezea kipato chake na kuwa na maisha mazuri zaidi.
. Atakuwa ameongeza pati la taifa kwa ujumla.
6. UWIWI.
Ni mdudu msumbufu wa maeneo ya nyanda za chini kwa hapa kwetu Tanzania. Hushambulia matunda na kuyachubua huku akifungamanisha matunda kadhaa kwa utando wa kahawia. Matunda hutobolewa na kukaushwa. Huweza pia kutoboa na kuharibu sehemu za juu zinazokua za matawi.
Kumdhibiti:
. Usafi wa shamba.
. Kukata matawi.
. Kuokota na kufukia matunda yaliyoharibiwa na yaliyofungamanishwa.
. Kuweka matandazo.
. Madawa yafaayo ni sawa na yale yaliyoainishwa kwa udhibiti wa kidomozi hapo juu.
7. BUNGUA NJANO.
Hushambulia majani hadi shina na kuathiri usafirishaji wa virutubisho, afya ya mti pamoja na mavuno. Dalili zake ni kunyauka sehemu za juu za matawi, matundu mengi madogo madogo kwenye tawi, matawi kuwa dhaifu na kuvunjika hasa kama yamezaa sana.
Kumdhibiti:
. Usafi wa shamba.
. Kuondoa matawi yaliyoathirika na kuyachoma au kuyafukia.
. Kuchokonoa matundu ya chini.
. Dawa asilia kama Utupa na Mwarobaini, na za viwandani kama Ultracide na Decis.
8. VITHIRIPI.
Hawa huweza kuwa tishio wakati wa ukame wa muda mrefu. Hushambulia sehemu zote laini za mmea (majani, vitawi vichanga na matunda) kwa kufyonza chembechembe hai. Majani yaliyoathirika yana rangi ya shaba juu na chini.
Kuwadhibiti:
. Usafi wa shamba.
. Kuweka matandazo, kivuli na kumwagilia maji ipasavyo.
. Piga dawa pale tu ukiona vithiripi watatu kwa jani. Waweza kutumia Selecron 50EC, millilita 50 kwa lita 15 za maji, utupa au mwarobaini.
Makala hii nimeiandaa kwa msaada wa kitaalam zaidi kutoka katika Taasisi ya uendelezaji na uboreshaji wa zao la kahawa Tanzania (TaCRI), kituo cha Mbimba- Mbozi, Mbeya.
Ahsanteni sana!
Imetayarishwa na kuandikwa na Marcodenis E. Misungwi- Agriculture Extension Field Officer at Mbozi District, Mbeya.
Sunday, March 2, 2014
UTUNZAJI WA VIFARANGA
Hebu tuanze kwanza na hatua ya kwanza kabla vifaranga havijafika.
UTAYARISHAJI WA BANDA.
1. Banda liwe safi
2. Pulizia dawa ya kuondoa viroboto, utitiri na chawa kwa kutumia Ectomin dip.
3. Dawa ya kudhibiti wadudu wasababishao magonjwa tumia disinfectant aina ya Vivid/ YH4.
4. Tayarisha taa na moto (charcoal) kwa ajili ya kuweka chumba kiwe na joto la kutosha.
Siku ya 1.
i) Vifaranga wanapofika tu wapewe Glucose kwenye maji kwa masaa 8 mfululizo. Baada ya masaa 4 ya mwanzo ya glucose wapewe pamoja na chakula.
ii) Baada ya hapo wapatiwe Vitalyte kwa siku 2 mfululizo.
Siku ya 3.
Wapewe chanjo ya Newcastle Vaccine kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo wapatiwe Vitalyte au Antisyress kwa diku 3 mfululizo.
Siku ya 7.
Wapewe chanjo ya Gumburo Vaccine kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo wapatiwe maji ya Antistress kwa siku 2 mfululizo.
Siku ya 10.
Wapatiwe OTC Plus kwa siku kwa saa 24 kwa siku 3 mfululizo.
Siku ya 14,18,19.
Wapatiwe Esb3 na Vitalyte kwa masaa 24 kwa siku 3 mfululizo.
Siku ya 21.
Wapewe Newcastle Vaccine kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo wapatiwe Antistress kwa siku 4 mfululizo.
Siku ya 28.
Wapewe Gumburo (booster) kwa masaa 2 mfululizo. Baada ya hapo wapatiwe Antistress kwa siku 2 mfululizo.
Siku ya 31.
Wapatiwe OTC Plus kwa siku 7 mfululizo.
Siku ya 43,44,45.
Wapatiwe Ecb3 na Vitalyte kwa masaa 24 mfululizo kwa siku 3.
Siku ya 50.
Wapewe chanjo ya Fowl Pox. Baada ya hapo endelea kuwapa Chickmycine au Chick Plus kwa wiki 2.
Siku ya 65.
Chanjo ya Gumburo na baada ya hapo endelea na Antistress.
Sku ya 69.
Wapatie dawa ya minyoo Levalap kwa siku 2 mfululizo.
Siku ya 72.
Wapatiwe Fluquin kwa siku 5 mfululizo.
Siku ya 79.
Wapatiwe Anticox na Vitalyte kwa siku 5 mfululizo.
Siku ya 90.
Wapewe tena chanjo ya Newcastle Vaccine kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo endelea kuwapa Antistress kwa siku 3 mfululizo.
Baada ya siku hizo 90, endelea kuwapa chanjo ya Newcastle kila baada ya miezi 3 pamoja na kuwapa tiba ya magonjwa mbalimbali yanayowakabili mara kwa mara. Pia tafuta ushauri kwa wataalan mara tu uonapo tatizo kwa kuku wako.
Ahsanteni sana na karibuni muweze kuelimika. Toa maoni yako.
Thursday, February 27, 2014
SEMINA ELEKEZI YA MIKOPO YA PEMBEJEO CHINI YA AGRA
Kwa kuliona hilo, watafiti (Researchers) kutoka katika kituo cha utafiti Uyole (ARI-Uyole) chini ya Mtafiti William Mmari wameweza kuja na mradi ambao unadhaminiwa (funded) na Agriculture Green Revolution for Africa, AGRA, chini ya mwenyekiti wake Koffii Annan. Mradi huu unafanya mambo mengi kwa mkulima huyu mdogo mdogo na kati ya mambo hayo ni "Mikopo ya Pembejeo kwa Wakulima". Mkulima anakopeshwa pembejeo ya kutosha kuhudumi ekari moja ama ya Mahindi au Maharage, kisha atarejesha mkopo huo wakati wa mavuno na riba kidogo ya uendeshaji ambayo si kubwa ya kumuumiza mkulima.
Katika kuongeza ufanisi wa mradi huo wa mikopo ya pembejeo kwa wakulima, ARI-Uyole wamewaita kuwapa mafunzo wataalam wa kilimo (Extension Officers) wa kata na vijiji vinavyoguswa na mradi kutoka katika wilaya za Mbozi na Mbeya vijijini. Mafunzo hayo yalichukua siku mbili yakilenga hasa kuzijua mbinu njia ambazo mkulima huyu aliyekopeshwa pembejeo aweze kuzalisha vizuri na kurudisha mkopo wote na yeye kubakiwa na ziada.
Washiriki walijifunza kwamba, ili mkulima aweze kuhudumia shamba vizuri, ni lazima ajiwekee akiba ambayo itamsaidia katika manunuzi ya pembejeo wakati wa kulima. Mkulima ashauriwe kujiunga na vikundi vya wakulima vya kuweka na kukopa kama, AMCOS, ambavyo kwa sasa vimesamba sana huko vijijini na wamiliki ni wakulima wenyewe.
Katika hali ya kawaida uzoefu unaonyesha kwamba, watu wengi wana fikra ya msaada (kusaidiwa) katika akili zao. Hili linadhoofisha sana Mikopo hasa hii ya Pembejeo. Ili kudhibiti hilo Mikopo ya Pembejeo ya AGRA inapitia kwa wanachama hai kwenye AMCOS na wataunda vikundi vidogo ndani mwao ili waweze kujisimamia.
Matarajio ya Mradi ni kumjengea uwezo mkulima ili aweze kujiendeleza mwenyewe na apanue kilimo chake.
Tuesday, February 18, 2014
MBOGA ZA MAUA: 2 BROKOLI.
Igawa zao lilistawishwa tangu zama za Warumi, ni katika karne hii tu ambapo limeenezwa na kutumiwa katika sehemu nyingi duniani. Kwa sasa mboga hii hustawishwa sana katika nchi nyingi za tropiki, hasa Afrika na Visiwa vya Caribbean.
Brokoli ina kiasi kikubwa cha Vitamini A. Sehemu inayotumiwa ni kichwa au ua la mmea ambalo kidogo hufanana na koliflawa. Tofauti kubwa ni kwamba tunda lake ni mkusanyiko wa vichwa au ni shada la maua madogo madogo yaliyokusanyika pamoja bila ya kubanana sana. Rangi ya matunda ni kijivu-kijani, au kibluu-kijani, au kijani iliyofifia. Brokoli huchukua muda mrefu zaidi kukua na kukomaa kuliko kabeji.
AINA: Kama yalivyo mazao mengine, pia kuna aina kadhaa za zao hili ambazo hupendelewa zaidi na wakulima au walaji, kwa mfano Calabrese, De Cicco, Texas 107, Carvet Hybrid, Barca Hybrid, Green Sprouting na Mountain.
Wakati wa kuvuna, ua lote hukatwa pamoja na sehemu ya juu ya shina ambayo ni laini. Vile vile unaweza kuongeza kidogo cha majani yazungukayo ua. Mapishi na matumizi yake ni sawa na ya kabeji au koliflawa; yaani huchemshwa na kutengenezewa mchuzi, au kufanywa supu na rojorojo.
USTAWISHAJI: Brokoli huweza kustawi katika sehemu ambazo koliflawa hustawi, lakini ina uwezo mkubwa zaidi wa kuvumilia joto na uhaba wa mvua. Ili kupata matunda makubwa, ni muhimu kuhakikisha kwamba matunda hayo yanavunwa nyakati za baridi. Hii ni kwa kuwa hali ya joto husababisha matunda kukua kwa haraka mno kiasi kwamba ni vigumu kufuata utaratibu wa kuyavuna kidogo kidogo na kwa wakati unaostahili. Hakikisha udongo hautepeti na kutuamisha maji. Unaweza kuongeza mavuno kwa kuweka mbolea ya Nitrogen (Sulphate of Ammonia).
MAGONJWA: Magonjwa na wadudu washambuliao zao hili ni sawa na wa kabeji na koliflawa.
KUVUNA: Kwenye sehemu za joto tunda la kwanza huvunwa siku 60-70 tangu kupandikizwa. Na kwa nyanda za juu, siku 100-120.
Ahsanteni!
Thursday, February 13, 2014
MBOGA ZA MAUA 1. KOLIFLAWA
Mmea wa koliflawa huweza kukaa bustanini kwa zaidi ya mwaka mmoja, lakini kwa kawaia hulimwa na kuvunwa kila mwaka. Kitumiwacho katika mmea huu ni kichwa au ua lake ambalo kidogo ni mviringo, jeupe na gumu. Wakati wa kukua ua au tunda hufunikwa na majani ya mmea. Ukubwa wa tunda hutegemea hali ya udongo na hewa, pamoja na aina ya mbegu. Tunda lake huliwa baada ya kuchemshwa, pia huweza kuachanganywa mboga nyingine au kwenye supu na achali.
Zipo aina nyingi za mboga hii ambazo hupendwa zaidi. Aina hizo hutofautiana kwa ukubwa wa mimea, ukubwa wa matunda, ugumu wake, umbo lake, muda wake wa kukomaa, wingi wa majani na kadhalika.
Miongoni mwa aina za koliflawa ambazo hujulikana zaidi ni: Early Patma, Early Maket, snowball, white Mountain, Kibo Giant, Southern cross.
Zao hili hupendelea hali ya baridi kiasi na unyevu mwingi. Hushindwa kuvumilia hali ya baridi sana au joto jingi. Katika sehemu zilizo na joto kali, matunda ya koliflawa huwa madogo mno, kwa hivyo, ni sehemu chache nchini mwetu ambako zao hili linaweza kustawi vizuri. Hata hivyo utafiti na majaribio yanaendelea kufanywa ili kuweza kupata aina zenye uwezo wa kustawi katika hali ya tropiki.
Koliflawa huchukua kiasi kikubwa sana cha chakula kutoka ardhini, hivyo licha ya kurudishia mbolea, pia baada ya kuvuna inashauriwa kupanda mimea isiyotumia chakula kingi, kama kunde, maharage.
Koliflawa huwa tayari kuvunwa baada ya majuma 10 hadi 18 tangu kupandikizwa bustanini. Muda wa kukomaa hutegemea aina ya mimea na hali ya hewa kwani huchelewa zaidi katika hali ya baridi sana. Matunda yavunwe kabla hayajalegea na kuanza kupoteza rangi yake.
Magonjwa yashambuliayo:
Damping Off, Black Rot, Stem Rot.
Ahsanteni sana.
Prepared by:
Marcodenis E. Misungwi
Agriculture Field Extension Officer.
Friday, January 31, 2014
MAGONJWA YA NG'OMBE.
I. MINYOO YA NG'OMBE.
Ugonjwa wa minyoo husababisha hasara kwa mfugaji wa ng'ombe . Utafiti unaonyesha kuwa ng'ombe wengi wanaathirika na minyoo hiyo hupunguza uzalishaji. Aidha utafiti unaonyesha kuwa tatizo la minyoo kwa ng'ombe limeenea hapa nchini kwetu.
(i) AINA ZA MINYOO.
Minyoo inayoathiri ng'ombe imegawanyika katika makundi mbalimbali kama ifuatavyo;
- Minyoo inayoishia kwenye maini ya ng'ombe (liverflukes).
- Minyoo inayoishia kwenye mapafu (lungworms).
- Minyoo mikubwa ya mviringo (large roundworms).
- Minyoo midogo ya mviringo (small roundworms).
(ii) MZUNGUKO WA MAAMBUKIZI.
Minyoo hupitia njia zifuatazo:
- Mnyama kuambukizwa na mwingine.
-Kupenya kwenye ngozi ya ng'ombe.
- Ndama kupata minyoo kupitia kwa mama (ng'ombe) alieathirika kwa minyoo wakati wa kuzaliwa.
- Ng'ombe kula mayai ya minyoo yaliyomo kwenye majani wakati wa malisho.
- Ndama kupata minyoo wakati wa kunyonya maziwa ya ng'ombe aliyeathirika.
(iii) DALILI ZA NG'OMBE ALIYEAMBUKIZWA.
- Kupoteza uzito
- Kukosa hamu ya kula
- Kuhara
- Kupungukiwa na damu
- Kuwa na homa
- Afya yake kufifia na hatimaye kufa
- Tumbo kuwa kubwa kupita kiasi (ndama).
(iv) TIBA
Wanyama wapewe dawa za kutibu minyoo mara kwa mara.
Mfano:
. NILZAN
. NILVERM
. PIPERAZINE
. ANACUR
. THIABENDAZOLE
. YOMESAN
. OXYDOZIDENE
(v) JINSI YA KUZUIA MAAMBUKIZI NA KUZUIA MINYOO ISIENEE.
Minyoo hukingwa kwa njia zifuatazo:
. Kuepuka kulisha ng'ombe kwenye majani yenye mayai ya minyoo.
. Ng'ombe wote wagonjwa watibiwe.
. Epuka kulisha na kunywesha kwenye mabwawa.
. Usafi wa banda uzingatiwe.
. Ng'ombe wasiruhusiwe kukanyaga malisho yao hasa kwenye zero grazing.
(vi) MADHARA YA MINYOO
. Husababisha upungufu wa damu.
. Husababisha upungufu wa maziwa.
. Ng'ombe huweza kufa.
II. UGONJWA WA MAPELE NGOZI
Mapele ngozi ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyojulikana kama Capripoxvirus. Virusi hivi huweza kukaa kwenye ngozi iliyokauka hadi siku 18.
Ugonjwa huu huwapata ng'ombe wa umri wowote, aidha virusi hivi hufa kwa muda mfupi katika kemikali mbalimbali kama ether 20% chloroform, farmalin 1% na phenol 2%.
A. JINSI MAPELE YANAVYOAMBUKIZWA.
Virusi vya mapele ngozi hupatikana kwenye mapele, mate na majimaji mengine ya mnyama mgonjwa. Ugonjwa huu unaambukizwa kwa kuumwa na mbu jamii ya Andes Culex baada ya kumuuma mnyama mwenye virusi.
B. DALILI ZA MAPELE NGOZI
Homa kali ambayo inaambatana na kutokea kwa mapele katika ngozi. Mapele haya yanaweza kuwa na ukubwa wa sentimeta 1 hadi 7 na huonekana katika sehemu ya kichwa, shingo, kiwele na miguuni. Mapele haya hukauka, kunyofoka na kuacha vidonda ambavyo huweza kushambuliwa na bakteria.
Mapele haya yanaweza pia kutokea katika mdomo. Dalili nyingine ni homa kali ya nyuzi joto sentigredi 40-41.5, mnyama hukosa hamu ya kula, kutoa machozi, kutokwa na makamasi mazito, kuvimba matezi, kupunguza uzalishaji maziwa na kutupa mimba. Baadae mapele hutokea mwili mzima.
C. JINSI YA KUZUIA MAPELE NGOZI.
Mapele ngozi unazuilika kwa kuchanja ng'ombe na kurudia chanjo mara moja kila mwaka ili kuongeza nguvu ya kinga. Zingatia kanuni zifuatazo:
. Ogesha mifugo kwa kutumia dawa ambazo zinaua wadudu ikiwa ni pamoja na mbu wanaoeneza magonjwa ya mifugo.
. Hamasisha wafugaji wengine kuchanja dhidi ya mapele ngozi na magonjwa mengine ya mifugo kama vile homa ya mapafu, ugonjwa wa miguu na midomo na ndigana kali.
. Toa taarifa kwa mganga wa mifugo aliyekaribu nawe unapoona dalili za ugonjwa huu ili hatua zinazopaswa zichukuliwe.
. Tenga wanyama wagonjwa na kuwapatia matibabu ya vidonda.
. Nunua ng'ombe kutoka eneo ambalo halina ugonjwa.
Kwa leo hebu tukomee hapa na tuweze kuhudumia mifugo yetu kwa ueasaha.
Ahsanteni!
Sent using a Sony Ericsson mobile phone
Thursday, January 30, 2014
Fw: UZALISHAJI BORA WA UYOGA.
---- Original message ----
From: Marcodenis <mmisungwi@gmail.com>
Sent: 30-Jan-2014 14:25
To: mgonga.misungwi@blogger.com
Subject: UZALISHAJI BORA WA UYOGA.
Uyoga ni zao la viumbe hai viitwavyo kuvu (fungi). Tanzania inao utajiri mkubwa wa uyoga wa asili. Uyoga wetu wa asili hupatikana wakati wa msimu wa mvua tu. Hili ni tatizo kubwa kwa vile wananchi walio wengi hupenda kula uyoga wakati wote.
Kwa sababu ya upatikanaji wa uyoga kwa msimu, na kwa vile aina nyingine za uyoga wa kienyeji zina sumu, tumefanya jitihada za kuanzisha kilimo cha uyoga ili kukidhi mahitaji ya wananchi kwa mwaka mzima. Pamoja na kutoa lishe bora kwa watu, uyoga pia unaweza kuzalishwa kama zao la biashara.
UMUHIMU WA ZAO LA UYOGA.
Uyoga kama chakula una viinilishe vingi vilivyo muhimu kwa afya ya binadamu. Uyoga una protini kati ya 3-4. Pia una vitamini B, C, D na K. Uyoga pia una madini yanayohitajika katika mwili wa binadamu.
Uynga ukitumika kama sehemu ya chakula cha familia mara kwa mara hutibu au kuzuia magonjwa kama vile saratani, vidonda vya tumbo, shinikizo la damu pia huongeza kinga ya mwili.
Kilimo cha uyoga huchangia pato la kaya na hutoa ajira. Kilimo hiki ni kizuri kwa wazee, akina mama na vijana kwa vile hakihitaji mtaji mkubwa kuanzisha na mavuno hupatikana baada ya muda mfupi. Aidha kilimo hiki hakihitaji eneo kubwa kama mawazo mengine kwani uyoga huoteshwa ndani ya banda.
MAHITAJI YA KUANZISHA KILIMO CHA UYOGA.
1. Mbegu
Kama mazao mengine; ili kuanzisha kilimo cha uyoga unahitaji mbegu. Maabara za mbegu za uyoga ziko Uyole hutoa aina mbalimbali za uyoga kwa bei ya nafuu.
2. Masalia ya mazao ya kilimo.
Kilimo cha uyoga hutumia masalia ya mazao ya kilimo kwa mfano majani ya mpunga, maharage, migomba, magunzi, mabua na ngano. Kwa ujumla kilimo cha uyoga hutunza mazingira kwa vile uchomaji wa masalia ya mazao ya kilimo huharibu mazingira.
Mabaki ya kilimo uyoga yanaweza kutumika kama mbolea, chakula cha mifugo au kuzalisha nishati ya gesi.
3. Banda.
Uyoga hulimwa ndani ya banda. Banda ligawanywe katika vyumba viwili, chumba chenye giza na chumba chenye mwanga na hewa. Banda liezekwe kwa nyasi (bati huleta tofauti ya joto kati ya mchana na usiku).
4. Kichanja au meza.
Kwa ajili ya kupozea majani na vifaa vya kupandia uyoga.
5. Pipa au sufuria kubwa.
Kwa ajili ya kuchemsha ili kuua wadudu na vimelea vya magonjwa kwenye masalia ya mazao ya kilimo.
6. Mifuko ya plastiki na kamba.
Uyoga hupandwa kwenye mifuko ya plastiki ambayo baada ya kupandwa hufungwa kwa kamba.
7. Hatua za kilimo cha uyoga.
- Fanya usafi kwenye banda la kulimia uyoga.
- Chambua masalia ya mazao ya kilimo (ondoa yenye rangi ya kijani) kisha osha kuondoa vumbi na uchafu mwingine.
- Weka maji theluthi moja ya chombo cha kuvukizia.
- Jaza vimeng'enywa kwenye pipa, funika na fukiza angalau kwa masaa mawili (tangu mvuke unavyotokea juu ya mfuniko).
- Ipua kwenye kichanja au meza iliyooshwa.
- Ikisha poa , angalia unyevu uliobaki kwenye vimeng'enywa kwa kukamua vimeng'enywa. Kama matone ya maji yanatoka; anza kupanda. Kama maji yanachuruzika bado kwa hiyo endelea kusambaza ili maji yatoke.
- Baada ya kunawa, sia kwenye mfuko wa plastiki tabaka ya vimeng'enywa ikifuatiwa na mbegu mpaka mfuko umejb. Mwishoni weka tabaka ya mbegu kisha funga mfuko kwa kamba.
- Toboa mashimo kama 8 kupitisha hewa juu, katikati na chini ya mfuko; kwa kutumia uma au kijiko.
- Weka mifuko kwenye chumba chenye giza ili mbegu ziote na utandu ufunike mfuko wote . Hii itachukua wiki 2-3 kutegemea na hali ya hewa.
- Hamisha mifuko kwenye chumba chenye mwanga na hewa ili uyoga uote.
- Uyoga utauta baada ya siku 7 mpaka 10. Vuna baada ya siku 4. Endelea kuvunaj mpaka mavuno yatakapofifia (baada ya miezi miwili hivi).
MATUMIZI
Tayarisha kama mboga zingine kwa kuunga na viungo. Pia unaweza kutengeneza supu ya uyoga, kuoka au kukaanga na kwenye vyakula vya 'mseto'. Uyoga wa zia