Mtandao huu ni kwa ajili ya kuelimishana juu ya Kilimo na Mifugo na changamoto zake. Karibu tujifunze wote.
Friday, January 31, 2014
MAGONJWA YA NG'OMBE.
I. MINYOO YA NG'OMBE.
Ugonjwa wa minyoo husababisha hasara kwa mfugaji wa ng'ombe . Utafiti unaonyesha kuwa ng'ombe wengi wanaathirika na minyoo hiyo hupunguza uzalishaji. Aidha utafiti unaonyesha kuwa tatizo la minyoo kwa ng'ombe limeenea hapa nchini kwetu.
(i) AINA ZA MINYOO.
Minyoo inayoathiri ng'ombe imegawanyika katika makundi mbalimbali kama ifuatavyo;
- Minyoo inayoishia kwenye maini ya ng'ombe (liverflukes).
- Minyoo inayoishia kwenye mapafu (lungworms).
- Minyoo mikubwa ya mviringo (large roundworms).
- Minyoo midogo ya mviringo (small roundworms).
(ii) MZUNGUKO WA MAAMBUKIZI.
Minyoo hupitia njia zifuatazo:
- Mnyama kuambukizwa na mwingine.
-Kupenya kwenye ngozi ya ng'ombe.
- Ndama kupata minyoo kupitia kwa mama (ng'ombe) alieathirika kwa minyoo wakati wa kuzaliwa.
- Ng'ombe kula mayai ya minyoo yaliyomo kwenye majani wakati wa malisho.
- Ndama kupata minyoo wakati wa kunyonya maziwa ya ng'ombe aliyeathirika.
(iii) DALILI ZA NG'OMBE ALIYEAMBUKIZWA.
- Kupoteza uzito
- Kukosa hamu ya kula
- Kuhara
- Kupungukiwa na damu
- Kuwa na homa
- Afya yake kufifia na hatimaye kufa
- Tumbo kuwa kubwa kupita kiasi (ndama).
(iv) TIBA
Wanyama wapewe dawa za kutibu minyoo mara kwa mara.
Mfano:
. NILZAN
. NILVERM
. PIPERAZINE
. ANACUR
. THIABENDAZOLE
. YOMESAN
. OXYDOZIDENE
(v) JINSI YA KUZUIA MAAMBUKIZI NA KUZUIA MINYOO ISIENEE.
Minyoo hukingwa kwa njia zifuatazo:
. Kuepuka kulisha ng'ombe kwenye majani yenye mayai ya minyoo.
. Ng'ombe wote wagonjwa watibiwe.
. Epuka kulisha na kunywesha kwenye mabwawa.
. Usafi wa banda uzingatiwe.
. Ng'ombe wasiruhusiwe kukanyaga malisho yao hasa kwenye zero grazing.
(vi) MADHARA YA MINYOO
. Husababisha upungufu wa damu.
. Husababisha upungufu wa maziwa.
. Ng'ombe huweza kufa.
II. UGONJWA WA MAPELE NGOZI
Mapele ngozi ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyojulikana kama Capripoxvirus. Virusi hivi huweza kukaa kwenye ngozi iliyokauka hadi siku 18.
Ugonjwa huu huwapata ng'ombe wa umri wowote, aidha virusi hivi hufa kwa muda mfupi katika kemikali mbalimbali kama ether 20% chloroform, farmalin 1% na phenol 2%.
A. JINSI MAPELE YANAVYOAMBUKIZWA.
Virusi vya mapele ngozi hupatikana kwenye mapele, mate na majimaji mengine ya mnyama mgonjwa. Ugonjwa huu unaambukizwa kwa kuumwa na mbu jamii ya Andes Culex baada ya kumuuma mnyama mwenye virusi.
B. DALILI ZA MAPELE NGOZI
Homa kali ambayo inaambatana na kutokea kwa mapele katika ngozi. Mapele haya yanaweza kuwa na ukubwa wa sentimeta 1 hadi 7 na huonekana katika sehemu ya kichwa, shingo, kiwele na miguuni. Mapele haya hukauka, kunyofoka na kuacha vidonda ambavyo huweza kushambuliwa na bakteria.
Mapele haya yanaweza pia kutokea katika mdomo. Dalili nyingine ni homa kali ya nyuzi joto sentigredi 40-41.5, mnyama hukosa hamu ya kula, kutoa machozi, kutokwa na makamasi mazito, kuvimba matezi, kupunguza uzalishaji maziwa na kutupa mimba. Baadae mapele hutokea mwili mzima.
C. JINSI YA KUZUIA MAPELE NGOZI.
Mapele ngozi unazuilika kwa kuchanja ng'ombe na kurudia chanjo mara moja kila mwaka ili kuongeza nguvu ya kinga. Zingatia kanuni zifuatazo:
. Ogesha mifugo kwa kutumia dawa ambazo zinaua wadudu ikiwa ni pamoja na mbu wanaoeneza magonjwa ya mifugo.
. Hamasisha wafugaji wengine kuchanja dhidi ya mapele ngozi na magonjwa mengine ya mifugo kama vile homa ya mapafu, ugonjwa wa miguu na midomo na ndigana kali.
. Toa taarifa kwa mganga wa mifugo aliyekaribu nawe unapoona dalili za ugonjwa huu ili hatua zinazopaswa zichukuliwe.
. Tenga wanyama wagonjwa na kuwapatia matibabu ya vidonda.
. Nunua ng'ombe kutoka eneo ambalo halina ugonjwa.
Kwa leo hebu tukomee hapa na tuweze kuhudumia mifugo yetu kwa ueasaha.
Ahsanteni!
Sent using a Sony Ericsson mobile phone
Thursday, January 30, 2014
Fw: UZALISHAJI BORA WA UYOGA.
---- Original message ----
From: Marcodenis <mmisungwi@gmail.com>
Sent: 30-Jan-2014 14:25
To: mgonga.misungwi@blogger.com
Subject: UZALISHAJI BORA WA UYOGA.
Uyoga ni zao la viumbe hai viitwavyo kuvu (fungi). Tanzania inao utajiri mkubwa wa uyoga wa asili. Uyoga wetu wa asili hupatikana wakati wa msimu wa mvua tu. Hili ni tatizo kubwa kwa vile wananchi walio wengi hupenda kula uyoga wakati wote.
Kwa sababu ya upatikanaji wa uyoga kwa msimu, na kwa vile aina nyingine za uyoga wa kienyeji zina sumu, tumefanya jitihada za kuanzisha kilimo cha uyoga ili kukidhi mahitaji ya wananchi kwa mwaka mzima. Pamoja na kutoa lishe bora kwa watu, uyoga pia unaweza kuzalishwa kama zao la biashara.
UMUHIMU WA ZAO LA UYOGA.
Uyoga kama chakula una viinilishe vingi vilivyo muhimu kwa afya ya binadamu. Uyoga una protini kati ya 3-4. Pia una vitamini B, C, D na K. Uyoga pia una madini yanayohitajika katika mwili wa binadamu.
Uynga ukitumika kama sehemu ya chakula cha familia mara kwa mara hutibu au kuzuia magonjwa kama vile saratani, vidonda vya tumbo, shinikizo la damu pia huongeza kinga ya mwili.
Kilimo cha uyoga huchangia pato la kaya na hutoa ajira. Kilimo hiki ni kizuri kwa wazee, akina mama na vijana kwa vile hakihitaji mtaji mkubwa kuanzisha na mavuno hupatikana baada ya muda mfupi. Aidha kilimo hiki hakihitaji eneo kubwa kama mawazo mengine kwani uyoga huoteshwa ndani ya banda.
MAHITAJI YA KUANZISHA KILIMO CHA UYOGA.
1. Mbegu
Kama mazao mengine; ili kuanzisha kilimo cha uyoga unahitaji mbegu. Maabara za mbegu za uyoga ziko Uyole hutoa aina mbalimbali za uyoga kwa bei ya nafuu.
2. Masalia ya mazao ya kilimo.
Kilimo cha uyoga hutumia masalia ya mazao ya kilimo kwa mfano majani ya mpunga, maharage, migomba, magunzi, mabua na ngano. Kwa ujumla kilimo cha uyoga hutunza mazingira kwa vile uchomaji wa masalia ya mazao ya kilimo huharibu mazingira.
Mabaki ya kilimo uyoga yanaweza kutumika kama mbolea, chakula cha mifugo au kuzalisha nishati ya gesi.
3. Banda.
Uyoga hulimwa ndani ya banda. Banda ligawanywe katika vyumba viwili, chumba chenye giza na chumba chenye mwanga na hewa. Banda liezekwe kwa nyasi (bati huleta tofauti ya joto kati ya mchana na usiku).
4. Kichanja au meza.
Kwa ajili ya kupozea majani na vifaa vya kupandia uyoga.
5. Pipa au sufuria kubwa.
Kwa ajili ya kuchemsha ili kuua wadudu na vimelea vya magonjwa kwenye masalia ya mazao ya kilimo.
6. Mifuko ya plastiki na kamba.
Uyoga hupandwa kwenye mifuko ya plastiki ambayo baada ya kupandwa hufungwa kwa kamba.
7. Hatua za kilimo cha uyoga.
- Fanya usafi kwenye banda la kulimia uyoga.
- Chambua masalia ya mazao ya kilimo (ondoa yenye rangi ya kijani) kisha osha kuondoa vumbi na uchafu mwingine.
- Weka maji theluthi moja ya chombo cha kuvukizia.
- Jaza vimeng'enywa kwenye pipa, funika na fukiza angalau kwa masaa mawili (tangu mvuke unavyotokea juu ya mfuniko).
- Ipua kwenye kichanja au meza iliyooshwa.
- Ikisha poa , angalia unyevu uliobaki kwenye vimeng'enywa kwa kukamua vimeng'enywa. Kama matone ya maji yanatoka; anza kupanda. Kama maji yanachuruzika bado kwa hiyo endelea kusambaza ili maji yatoke.
- Baada ya kunawa, sia kwenye mfuko wa plastiki tabaka ya vimeng'enywa ikifuatiwa na mbegu mpaka mfuko umejb. Mwishoni weka tabaka ya mbegu kisha funga mfuko kwa kamba.
- Toboa mashimo kama 8 kupitisha hewa juu, katikati na chini ya mfuko; kwa kutumia uma au kijiko.
- Weka mifuko kwenye chumba chenye giza ili mbegu ziote na utandu ufunike mfuko wote . Hii itachukua wiki 2-3 kutegemea na hali ya hewa.
- Hamisha mifuko kwenye chumba chenye mwanga na hewa ili uyoga uote.
- Uyoga utauta baada ya siku 7 mpaka 10. Vuna baada ya siku 4. Endelea kuvunaj mpaka mavuno yatakapofifia (baada ya miezi miwili hivi).
MATUMIZI
Tayarisha kama mboga zingine kwa kuunga na viungo. Pia unaweza kutengeneza supu ya uyoga, kuoka au kukaanga na kwenye vyakula vya 'mseto'. Uyoga wa zia
Saturday, January 25, 2014
MAGONJWA MUHIMU YA KUKU
1. Ugonjwa wa Mdondo (Newcastle Disease)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi, huathiri mifumo ya fahamu, chakula na upumuaji. Mara nyingi huwapata kuku wakubwa wa umri miezi 5-8.
Dalili za ugonjwa
- Vifo vingi vya ghafla.
- Mharo wa kijani na wakati mwingine ukiwa na damu.
- Macho na koo hujaa maji.
- Kunyonga shingo.
TIBA: Ugonjwa huu hauna tiba.
KINGA: Chanja siku ya kwanza hadi ya tatu baada ya kuanguliwa kisha na urudie kuwachanja baada ya wiki 3-4. baada ya hapo, kila baada ya miezi 3.
Zuia uingiaji wa watu, kuku, wageni au vifaa kwenye banda hasa toka kwenye maeneo yenye maambukizo.
Wapewe antibiotics i.e Doxycol, Fluban, OTC 20% na Vitastress na Amprolium kuzuia magonjwa nyemelezi.
2. Ndui ya kuku (Fowl Pox)
Ugonjwa huu unasababishwa na kirusi ambaye huenea taratibu na kusababisha upele kwenye kishungi, ngozi na mfumo wa hewa. Huwapata kuku wa umri mbalimbali.
DALILI
- Upele kwenye ngozi ya shingo na maeneo mengine yasiyo na manyoya kama miguu, na sehemu ya kutolea kinyesi.
- Vipele hupasuka na kufanya gamba gumu (scab)
- Utando mdomoni/puani unaoambatana na mafuta.
- Vipele vya puani humfanya kutoka majimaji puani.
- Vipele vya machoni husababisha kutoka kwa machozi.
- Maambukizi ni ya taratibu lakini vifo hutokea hadi 50%.
TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba. Kuku wapewe vitamin ili kuwaongezea hamu ya kula. Kuku wapewe viuavijasumu (antibiotics) i.e OTC 20% kuzuia magonjwa nyemelezi.
KUZUIA
Kuku wapatiwe chanjo ya ndui. Chanjo hutolewa kwenye maji ya kunywa ama kuchomwa sindano kwenye bawa.
CHANJO
Chanjo itolewe mara mbili kama ifuatavyo:-
(i) Kati ya siku 5-26 (wastani wa umri wa wiki 4)
(ii) Chanjo ya pili itolewe mwezi (1-2) kabla ya kuku kuanza kutaga.
Friday, January 24, 2014
SHAMBANI SOLUTIONS: ICT ADVANCEMENT SHOULD HELP FARMERS PRESS AHEAD
Saturday, January 18, 2014
KULISHA KUKU WA ASILI
Walishwe chakula chenye mchanganyiko wenye virutubisho vyote muhimu ambavyo ni:-
(i) Vyenye asili ya wanga mfano mahindi, pumba, mtama n.k
(ii) Vyenye asili ya protini mfano dagaa, soya, mashudu, damu n.k
(iii) Vyenye asili ya madini mfano mifupa iliyosagwa, chokaa, premix ya kuku n.k
(iv) Vyenye asili ya vitamini mfano mboga mboga, vitamini maalumu zinazopatikana madukani.
Kiwango cha kila kiinilishe ni lazima kizingatiwe ili kuku aweze kupata uwiano sawa wa viinilishe swala ambalo ni muhimu katika uzalishaji wake. Michanganyiko hii inaweza kutumika ama kuboresha kulingana na upatikanaji wa vyakula hivyo.
Katika kutengeneza chakula cha kuku mfugaji lazima kwanza azingatie kiasi cha protini na wanga na uwiano wake. Protini inayotolewa lazima izingatie ubora wake katika viasili hivi yaani LYSINE, METHIONINE na CYSTINE. Pia chakula lazima kizingatie kiwango cha madini hasa CALCIUM na PHOSPHORUS na mahitaji ya vitamin. Baada ya kujua haya mfugaji anaweza kutengeneza chakula chake mwenyewe. Kiwango cha vitamini D ni muhimu sana kwa matumizi ya madini ya calcium na phosphorus.
Uchanganyaji wa chakula cha kuku kwa makundi yote:
Protini 25%
Mimea 18-22%
Wanyama 5-8%
Wanga 68%
Pumba za mahindi 60-68%
Madini 7%
Calcite 5%
Madini maalumu (standard mineral mixture) 2-3%
Vitamini (premix)- hii inategemea maelekezo ya mtengenezaji.
Hebu tuangalie sasa uwiano wa uchanganyaji:
- Pumba za mahindi 66kg
- Mashudu ya alizeti 18kg
- Dagaa 7kg au (4kg Dagaa 3 Damu), 4 dagaa 3 soya)
- Mifupa iliyosagwa 5kg
- Chokaa 2kg
- Madini/vitamini maalumu 2kg
Jumla ya mchanganyiko ni 100kg kwa uwiano.
Lakini pamoja na ulishaji huo kwa kuku, mfugaji hana budi kufuata na kutekeleza ratiba ya kuzuia magonjwa (Chanjo) na kutoa tiba sahihi ugonjwa unapotokea.
Ahsanteni!
HAPPY NEW YEAR!
Thursday, January 16, 2014
KILIMO BORA CHA VITUNGUU.
Kuotesha mbegu katika kitalu
Tengeneza matuta yenye upana wa mita 1 na urefu wowote kutegemea na mahitaji yako.
Weka mbolea ya samadi ndoo moja hadi mbili kwa mraba wa mita moja.
Lima tuta kiasi cha sentimita 10-25.
Sia mbegu katika mistari yenye nafasi ya sentimita 15 kutoka mstari hadi mstari. Gramu 5 (kijiko cha chai) zinatosha kusia eneo la mraba mita moja.
Tandaza nyasi na mwagilia.
KUMBUKA: Kilo 2.5 za mbegu zinatosha hekta moja ya shamba.
KANUNI YA PILI
Kupanda miche kwa nafasi.
Pandikiza miche katika nafasi ya sentimita 30 kutoka mstari na mstari na sentimita 10-25 toka mche hadi mche.
KUMBUKA: Pandikiza miche wakati wa asubuhi au jioni na mwagilia maji ya kutosha.
KANUNINI YA TATU
Weka mbolea.
Weka mbolea ya kukuzia katika wiki ya nne hadi sita baada ya kupandikiza. Weka mbolea kwenye mstari na hakikisha isigusane na mimea. Hakikisha udongo una unyevu wa kutosha wakati wa kuweka mbolea. Tumia UREA au SA.
KANUNI YA NNE
Kupalilia
Hakikisha shamba linakuwa safi. Wakati wa kupalili, mkulima asichimbue sana udongo ili kuepuka mikwaruzano kwenye shina la vitunguu. Inulia udongo kwenye mashina kama mkulima amepanda sesa.
KANUNI YA TANO
Kuzuia magonjwa/wadudu
Magonjwa ya ukungu ni magonjwa yanayoishambulia mimea ya vitunguu. Magonjwa hayo ni Down Mildew, ugonjwa wa kuvu, kuoza kwa vitunguu.
KUZUIA
Tumia dawa zenye mchanganyiko wa copper mfano Dithane m45, Ivory na Koside. Epuka mikwaruzo/vidonda kwenye vitunguu na pia fuata kanuni za mzunguko wa mazao (crop rotation).
Wadudu waharibifu:
Wadudu wa manjano (Onion thrips). Zuia wadudu hawa kwa kutumia dawa za viwandani kama Actellic 50EC, Selecron na pia madawa ya wadudu yanayopatikana kwenye maduka.
KANUNI YA SITA
Kuvuna kwa wakati
Vuna vitunguu baada ya miezi 4-5 kutegemeana na mbegu iliyopandwa.
Ucheleweshaji wa uvunaji unasababisha vitunguu kuoza na kuharibikia shambani.
KUMBUKA: Tumia jembe la mkono na hakikisha vitunguu havikwaruzwi wakati wa kuvuna. Mkulima anaweza kuvuna tani 30-40 kwa hekta.
HAPPY NEW YEAR!
Saturday, January 11, 2014
UJUE UTUPA NA KAZI ZAKE
MATUMIZI YA UTUPA.
(i) Kufukuza Panya/ Mchwa.
Mti huu husaidia kuondoa wadudu na wanyama waharibifu wanaokaa ardhini. Panda Utupa 3m kila upande (3m * 3m) na mpakani mwa shamba lako, baada ya mwaka mmoja shamba lako litakuwa halina mashimo ya Panya. Kama kichuguu cha Mchwa panda mmea huu karibu na kichuguu na baada ya mud kitakufa.
(ii) Kuogesha Mifugo
Chukua kilo 1 ya majani ya Utupa na Maji lita 25, loweka kwa masaa 4 hadi 6 au chemsha kwa dakika 30 na lita 27 za maji, chuja kwa kitambaa, kisha osha mifugo yako.
Changanya na sabuni ya unga kidogo dawa iweze kunata na kukaa kwenye ngozi ya mnyama.
ONYO: Usitumie majani ya Utupa kuogeshea Nguruwe, hawana uwezo wa kuhimili dawa hii kwenye ngozi zao.
(iii) Kunyunyizia shambani.
Chukua kilo 1 ya Majani ya Utupa na maji lita 5, loweka kwa masaa 10 hadi 16 kisha chuja na weka kwenye bomba, tayari kwa kupulizia shambani. Ina uwezo wa kuua aina ya wadudu wote shambani.
(iv) Kuhifadhi Nafaka ghalani.
Pima gramu 100 za unga wa majani ya Utupa, changanya na Mahindi au Maharage kilo 100. Dawa hii huwa na nguvu kwa muda wa mwaka mzima.
Kwa wale wenye mashamba ya kahawa ni vema na muhimu sana kupanda Utupa kuzunguka mashamba yenu na kama shamba ni kubwa sana unaweza panda na katikati ya shamba pia. Faida nyingine ya mmea huu, hurutubisha udongo maana ni jamii ya mikunde.
Ndugu zangu wakulima, nawashauri muanze sasa kupanda Utupa shambani na nyumbani pia.
Ahsanteni!
Happy New Year.
Thursday, January 2, 2014
NDIGANA BARIDI, UGONJWA HATARI KWA MIFUGO.
JINSI UGONJWA HUU UNAVYOAMBUKIZWA (Mode of transmission of the disease)
Ugonjwa wa ndigana baridi unaambukizwa kupitia kwenye ng'ombe mgonjwa baada ya kuumwa na kupe, mbung'o au inzi, aina ya ng'ombe, mbuzi au kondoo walio na afya nzuri ili kupata chakula yaani kunyonya damu wakati wananyonya damu pia ng'ombe asiye mgonjwa. Pia kwa njia ya kutumia vifaa vya kitaalamu ambavyo havikuchemshwa sawasawa kama sindano, vijidudu vya ugonjwa husambazwa kutoka mnyama mgonjwa kwenda mnyama mwenye afya kwa kutumia vifaa hivyo.
Hivyo uangalizi mkubwa unatakiwa wakati shughuli hizo za kuchoma sindano, kukata pembe n.k. zinapofanyika.
WANYAMA WANAOPATA UGONJWA WA NDIGANA BARIDI.
- Ng'ombe
- Mbuzi
- Kondoo
Ndama wadogo hawapatwi na ugonjwa huu.
DALILI KUU ZA UGONJWA.
Dalili kuu za ugonjwa huu ni:-
(i) Homa kali (40-41C).
(ii) Kinyesi kigumu sana na chenye utando mweupe juu yake.
(iii) Kupumua/kuhema kwa shida.
(iv) Mnyama kushindwa kucheua.
(v) Rangi ya njano mdomoni, puani na sehemu zilizo wazi za mnyama kama machoni n.k.
(vi) Kukosa hamu ya kula.
(vii) Kupunguza uzalishaji wa maziwa.
(viii) Kutokunywa kwa sababu ya omasum kutofanya kazi (constipation).
MAGONJWA MENGINE YANAYOFANANA NA NDIGANA BARIDI.
-Ndigana kali
-Kuvimbiwa (bloat)
-Kichomi
JINSI YA KUZUIA UGONJWA WA NDIGANA KALI.
-Hakikisha wanyama wako wanaogeshwa vizuri na dawa ya kuua kupe (Acarcides)
-Ogesha kwa kutumia dawa zinazozuia kupe na mbung'o mara 1 kwa wiki mfano Tristix, Tixfix, Ciberdip, Paranex, Alfanex, Steladone, Dominex n.k.
-Chunga mifugo yako katika mbuga zisizo na kupe au mbung'o.
-Ikiwezekana chunga/lisha kwa mzunguko (rotational grazing) katika mbuga zako ili kupunguza kuzaliana kwa kupe.
JINSI YA KUTIBU MNYAMA MWENYE NDIGANA BARIDI
-Watibiwe kwa kutumia dawa ya Oxytetracycline ya sindano 5-10mg/kg ya uzito
-Wanyama waliofunga choo wanyweshwe mafuta ya kupikia ili kulainisha tumbo
Ahsanteni!igana

